Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki Nyongeza ya Tano ya Mwaka 1994, Itifaki Nyongeza ya Sita ya Mwaka 1999, Itifaki Nyongeza ya Saba ya Mwaka 2004, Itifaki Nyongeza ya Nane ya Mwaka 2008 na Itifaki Nyongeza ya Tisa ya Mwaka 2016 ya Katiba ya Umoja wa Posta Duniani

Hon. Prof. Makame Mnyaa Mbarawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkoani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki Nyongeza ya Tano ya Mwaka 1994, Itifaki Nyongeza ya Sita ya Mwaka 1999, Itifaki Nyongeza ya Saba ya Mwaka 2004, Itifaki Nyongeza ya Nane ya Mwaka 2008 na Itifaki Nyongeza ya Tisa ya Mwaka 2016 ya Katiba ya Umoja wa Posta Duniani

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nawashukuru sana Wabunge wote kwa kuelewa umuhimu wa Itifaki hizi kwa maslahi ya Shirika la Posta Tanzania vilevile kwa maslahi ya nchi yetu. Kama tunavyojua sasa kwamba kumekuwa na mabadiliko makubwa ya teknolojia na utandawazi kwa hivyo ni muhimu sana kuwa tunaendana na mabadiliko haya kuhakikisha kwamba nchi yetu haiachwi nyuma katika maendeleo vilevile nchi yetu inaendelea vizuri na kuhakikisha tunatoa huduma nzuri za posta ambazo tunahitaji sana hasa katika kipindi hiki.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumepokea baadhi ya mapendekezo ya Kamati ya Miundombinu ambayo ndiyo Kamati Mama kwenye sekta yetu hii na tunawahakikishia tu Wajumbe wote wa Kamati hii kwamba maoni yao yote waliyotoa hasa kwenye upande wa anuani za makazi na
misimbo ya posta tutazifanyia kazi kwa maslahi ya nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaamini kabisa kama nchi yetu itaweza kuweka mifumo ya anuani za makazi na misimbo ya posta, bila shaka tutaweza kupeleka uchumi wetu mbele hasa ukiangalia kwamba tutakuwa na uwezo mkubwa wa kuweza kumtambua mtu kila alipo na tukifanya hivyo tutaweza kulipa kodi vizuri, tutaweza kuokoa wananchi pale tunapokuwa na majanga na tunaweza kuutumia mfumo huo ukatusaidia kwa kiasi kikubwa kuleta maendeleo yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nawashukuru tena kwa kukubali kupitisha Maazimio yetu ya Itifaki kuanzia ya Tano ya mwaka 1994, Itifaki Nyongeza ya Sita ya mwaka 1999, Itifaki Nyongeza ya Saba ya mwaka 2004, Itifaki Nyongeza ya Nane ya mwaka 2008 na Itifaki Nyongeza ya Tisa ya mwaka 2016.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kutoa hoja.