Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Uanzishwaji wa Kamisheni ya Pamoja ya Bonde la Mto Songwe kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Malawi pamoja na Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Amani na Usalama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Hon. Ester Michael Mmasi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Uanzishwaji wa Kamisheni ya Pamoja ya Bonde la Mto Songwe kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Malawi pamoja na Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Amani na Usalama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

MHE. ESTER M. MMASI: Mheshimiwa Naibu Spika, nina heshima ya pekee kusimama kwenye Bunge lako Tukufu nami kuweza kuchangia kwa kifupi sana kuhusiana na documents hizi tatu ambazo tumeletewa, tuweze kuzipitia kwa minajili ya kuweza kulinda na kuhifadhi maliasili ya Tanzania, kuweza kulinda amani na usalama wa nchi yetu na kuinua uchumi wa Tanzania kupitia mradi wa Hoima - Tanga.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitajielekeza tu kwenye Azimio hili moja la mkataba kuanzisha Kamisheni ya Pamoja ya Bonde la Mto Songwe, kwa sababu kimsingi sikuweza kupitia documents zote.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikianza kabisa na kurasa ya saba Article No. 7, uundwaji wa hii Council, tukisoma pale Section (1) tunasema kwamba Board Members watakaoiunda hii Council, tume-mention kwamba hatutakuwa na zaidi ya watu sita.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia katika watu sita, tuka- mention relevant Ministries ambazo tunafikiri zitatengeneza hii Board Composition kwenye kusimamia hii Council. Pia tuka-mention Wizara ya Maji, Ardhi, Energy, Irrigation, Agriculture and Local Government. Katika hawa watu sita, ukiangalia hizi Wizara hapa, tunapata watu watano, lakini hii nafasi moja tumeacha kwenye discretion power ya nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nafikiri pengine ni vizuri Wizara ikajaribu kuangalia au ku-consider technical personell ambaye ana specified background ya finance au accounting management.

Mheshimiwa Naibu Spika, nasema hivyo kwa sababu ukiangalia kwenye majukumu haya ya hii Bodi, utaona pale kwenye page eight Section (c), tunasema kwamba pamoja na majukumu mengine hii Council itakuwa na majukumu ya: “to establish guidelines for financial and technical assistance and development of projects and programs.” Pia ukienda
(d) tunasema kwamba, pamoja na majukumu mengine, hii Council itakuwa na majukumu ya ku-approve the budget of the Commission by the joint Steering Committee and such blah blah blahs.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, concern yangu, nafikiri ni vyema kwa kuwa tume- consider Deputy Ministers ndio ambao watatengeneza hii Council, kwenye nafasi za watu sita tume consider Deputy Minister’s watano. Ni concern yangu kwamba pengine either tu-consider na Deputy Minister from the Ministry of Finance ama tuwe specified tuseme kabisa tutahitaji kuwa na technical personnel mwenye specified background in financing or accounting. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, siyo hivyo, nikija page nine, kwenye the Committee; uundwaji wa hiyo committee, ukisoma pale Section One inasema kwamba hiyo Committee itaundwa na Wajumbe watano, lakini hatujaona background of the relevant Ministries ambao wataunda hii Committee kama ambavyo ilikuwa kwenye Council.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ni ushauri wangu pia tuseme hawa members wana background gani; au watatoka kwenye Bodi gani; au ni Ministries gani? Tusiache tu hivyo ina-hang. Kismsingi naona kama vile tunahitaji kuongeza kitu hapo.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia ukija pale the Chairmanship of the Committee, tumesema kwamba huyu Chairman atakuwa anaishi kwenye nafasi yake kwa muda wa mwaka mmoja na itakuwa ina-rotate, lakini pia nikawa nahoji ni vyema basi tungeona the life span au project duration kwa maana kwamba mimi ningeweza kusema mbona one year haitoshi? Sasa napata shida kwa sababu hata sijui life span ya hii project, yaani the Shared Watercourse Projects. Kwa hiyo, ni vyema basi tukaona kabisa hii project ni ya muda gani?

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kimsingi naona hivyo, kwa sababu naweza nikasema kwamba mwaka mmoja hautoshi au nikashindwa kupata relevance ya mwaka mmoja kwa sababu kimsingi sijui hata life span ya hii project. Kwa hiyo, concern yangu kwenye section hiyo ilikuwa ni hiyo niliyoi-mention.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nikienda section 12 kwenye Sekretariet, tunasema pamoja na Bodi itakayoteuliwa; appointing authority of cource imekuwa mentioned, lakini pia tukasema itakuwa headed na Executive Secretary pia itakuwa assisted na Deputy Executive Secretary lakini who are the body? Hatujaona bado hii bodi ni akina nani? Wako wangapi? Wanatoka wapi?

Mheshimiwa Naibu Spika, pia ukiangalia functions, it means zinatakiwa ziwe performed na a certain number of people, lakini siyo tu Executive Secretary au Deputy Secretary. Kwa hiyo, kimsingi naona tuna haja kabisa ya kusema idadi ya Board Members, ikibidi pia na background zao, lakini siyo tu kusema kwamba itakuwa headed na nani kwa sababu tayari tuna duties and responsibilities to be performed by a certain number of people.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimejaribu kwenda kwa haraka haraka page number 15, kuhusu dispute resolution. Ukiangalia kwenye hii dispute resolution, the way imekuwa drawn, hutaona who is the specified body to deal with the disputes or misunderstandings. Nadhani ingekuwa ni muhimu kabisa na itakuwa na tija kama tutaweka the governing board ya kuweza ku-overseas disputes au misunderstandings.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakumbuka mpaka Ziwa Malawi, ile misunderstanding ambayo tuliyokuwa nayo, nafikiri ni fundisho tosha. Kwa hiyo, kimsingi napenda kabla ya ku-question kwa nini SADC Tribunal iwe ndiyo Appellate Board lakini pia ni muhimu tukaona kwamba kunakuwa na governing board ya ku-overseas any dispute that may arise during the execution of this project.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia ukisoma hii document inakwambia host country ni Tanzania na Makao Makuu yatakuwa Mbeya kule Songwe. Sasa kama host country ni Tanzania, kwa nini Appellate Board inabaki kuwa SADC Tribunal? Kimsingi niki-refer hata kuna Mjumbe mmoja ameongea humu ndani, lakini siangalii kwake, naangalia kama nilivyoelewa.

Mheshimiwa Naibu Spika, tulipitisha hapa juzi Miswada ya kuweza ku-govern our natural resources, ile Permanent Sovereignty Act ambayo tulijikita na tukasema kabisa kwamba any dispute or misunderstands zitakuwa dealt within the country. Kimsingi ukiangalia hii document na ukiangalia vitu ambavyo tumepitisha Miswada na Sheria ambazo tumepitisha nadhani hapa kunaleta ukakasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, niseme tu kwamba naunga mkono hoja asilimia mia, mawasilisho yaliyoletwa na Wizara husika katika muktadha mzima wa kuijenga Tanzania yenye uchumi wa kati, lakini pia ni subject to minor corrections where necessary. Ahsante sana.