Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Uanzishwaji wa Kamisheni ya Pamoja ya Bonde la Mto Songwe kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Malawi pamoja na Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Amani na Usalama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Hon. Masoud Abdalla Salim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtambile

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Uanzishwaji wa Kamisheni ya Pamoja ya Bonde la Mto Songwe kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Malawi pamoja na Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Amani na Usalama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Mheshimiwa Naibu Spika, nitaongea dakika nane na Mheshimiwa Bobali ataongea dakika saba.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Nami nitajielekeza kwenye Azimio moja tu ambalo ni Azimio la Kuridhia Itifaki ya Amani na Usalama ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (East African Community Protocol on Peace and Security). Katika muktadha wa shughuli nzima za ulinzi na usalama na jinsi ambavyo articles zilivyokuja, naomba nianze na Article 12 ambayo inasema combating trans-national and cross border crimes. Katika mambo ambayo yameelezwa, sitaki nisome sentensi zote lakini nataka niende kwenye ile
(e) illegal migration (uhamiaji haramu).

Mheshimiwa Naibu Spika, katika dhana nzima hii ya uhamiaji haramu, imeonekana kwamba wakati tukiweza kupitia Azimio hili kuridhia Azimio hili, naunga mkono Azimio hili lakini tuangalie ni kwa jinsi gani kwa muda mrefu, pamoja na vipengele vilivyomo katika Azimio hili, vya kuweza kuchukua taratibu, sheria na kanuni, lakini tuangalie ni kwa nini baadhi ya wahamiaji haramu wanaotoka Eritrea, Ethiopia, Somalia wanafika kwetu Tanzania ilhali wanapita katika nchi ya Kenya.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna mambo hapa ya kujifunza, tunataka kwenda katika utaratibu ambao tunataka kwenda vizuri na wenzetu kuona kwamba kuna hatua ambazo zitachukuliwa, kuna mikakati ambayo itafanywa, lakini wasiwasi ambao unakuja hapa sasa ni mahusiano, maelewano ya ziada katika shughuli nzima ya kutoka wahamiaji haramu kutoka Eritrea, Ethiopia, Somalia wanaopita Kenya kuja kwetu. Naomba hilo liwe angalizo kubwa katika mkataba wetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nenda katika Article 13; preventing and combating cattle rustling, ule wizi wa mifugo. Katika shughuli nzima hii ya wizi wa mifugo kumekuwa na operesheni nyingi sisi wenyewe kwanza hapa. Tulikuwa na Operesheni Tokomeza ambayo ukiangalia Ukanda ule wa Kigoma kulikuwa na mambo mengi, lakini katika maeneo mengine ambayo viongozi hasa wa mipakani walio katika maeneo yale ya wafugaji, wamekuwa wakipata matatizo sana na malalamiko sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kabla ya kutekeleza itifaki hii na kuiridhia inaonekana viongozi walioko mipakani, Watendaji wa Vijiji, Viongozi wa Chama, sisemi ni chama gani lakini inaonekana wale walio wengi zaidi kwa sababu ndio waliopata ushindi katika maeneo haya wengi wanapata, chama hicho, sitaki kutaja kwa sababu nikitaja itakuwa ni ukakasi, wataanza mambo ya hapa na pale lakini hili ni tatizo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Viongozi hawa wanapokea rushwa, viongozi hawa ndio wanaoingiza mifugo, tumesema mara nyingi lakini bado Serikali imekuwa ikisema kwamba itachukua hatua hii, utaratibu unakwenda, tuna mipango kabambe, mikakati hapa na pale, lakini hakuna kitu. Hilo ni tatizo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunakwenda kuridhia mkataba huu, mimi sina pingamizi nimesema naunga mkono kabisa, lakini tuangalie jambo lingine, tunakwenda kuridhia itifaki hii, lakini tuna tatizo kubwa la urejeshaji wa alama za mipaka (beacons). Hili suala ni la ulinzi na usalama, amani na utulivu. Mheshimiwa Shamsi anajua, Mheshimiwa Hussein Mwinyi anajua na wengine wanajua. Tuna tatizo kubwa la urejeshaji wa mipaka katika maeneo mbalimbali, ripoti kadhaa zimesema kwamba baina ya Tanzania pale Tarime na Migori Kenya beacons zimeondolewa kwa muda mrefu, Serikali inasema tuna mkakati, suala hili ni mtambuka, itachukuliwa hatua hapa na pale, hakuna kitu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tumetaja maeneo, kuna Vijiji vya Panyakoo, Ronche, Ikoma, leo kila wakati unasikia kwamba beacons zimeng’olewa, zimeondolewa, lakini utaratibu maalum haupo. Sasa tunakwenda kwenye Itifaki hii lakini kuna mambo sisi wenyewe kwanza kwa kuwa mambo haya ni mtambuka, Wizara ya Ulinzi, Wizara ya Mambo ya Ndani, TAMISEMI, Mambo ya Nje, zote tukae kwa pamoja katika nchi hizo husika wakati tunakwenda kuridhia itifaki hii kuweka utaratibu wetu, hili jambo likae vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, maana inaonekana kama tunasukumwa tu, kwanza tumechelewa. Tangu tarehe 12, Machi iliposainiwa tumekaa miaka minne, tumebakia sisi na Burundi tu, sisi Watanzania ni watu wa mwisho tu, kuna mambo kidogo ya kujifunza hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mambo haya ambayo tunakwenda nayo, basi napenda kusema kwamba Msemaji wa Kambi ya Upinzani alisema kwamba ni vema nchi zetu za Kiafrika ziendelee kujifunza katika kudumisha amani na utulivu katika mambo ya demokrasia pale ambapo mmoja kashindwa akubali matokeo. Unafuta uchaguzi, kwa nini ufute uchaguzi? Kwa mantiki ipi, kwa dhana ipi? Kwa manufaa ya nani? Umeshindwa kaa pembeni kwa sababu hakuna mwenye hatimiliki ya kuongoza, nchi ni yetu sote.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo amesema Msemaji wa Kambi ya Upinzani, namshukuru sana Msemaji, Mheshimiwa Cecilia Paresso, amesema jambo kubwa kweli, jambo zuri, jambo jema, amewaambia kwamba katika kudumisha amani na utulivu katika demokrasia hizi za mfumo wa Vyama vingi pale ambapo mmoja atashindwa basi akae pembeni, ni jambo jema sana, na hili tupate kujifunza katika maeneo mbalimbali.(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya hayo machache, bila kupigiwa kengele ile ya mwisho, nashukuru sana na naunga mkono Azimio hili la Amani na Usalama, lakini amani iwe ya kweli, isiwe ile amani ya kuigiza igiza.