Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Naibu Spika, nachangia Wizara hii kama ifuatavyo:-

Kwanza, bajeti iliyotengwa katika Wizara hii haitoshi, Serikali iongeze fedha katika Wizara hii; pili ni kuhusu maombi ya fedha kwa ajili ya Muze Group. Mheshimiwa Naibu Waziri maombi ya mradi huu ni maombi ya kupeleka maji ya mserereko toka chanzo cha Mto Kalumbaleza na mradi huu unatarajiwa kupeleka maji katika vijiji kumi na mbili, kwa nini mradi huu haujatengewa fedha?

Tatu, miradi ya umwagiliaji tumekuwa tukiiombea pesa mfululizo miaka mitano hatujawahi kupewa, tatizo ni nini? Mradi wa umwagiliaji wa Maleza, mradi wa umwagiliaji wa Uzia na mradi wa umwagiliaji wa Msia. Naomba maelezo kwa nini Serikali haitoi pesa katika miradi hiyo ya umwagiliaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.