Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana na ninawapongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na watendaji wote. Nitazungumzia maeneo mawili tu, kwanza utunzaji wa vyanzo vya maji na uvunaji wa maji ya mvua.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninasisitiza Serikali izidi kutoa elimu kwa wananchi kuhusu utunzaji wa vyanzo vya maji, narejea kitabu cha hotuba ya Mheshimiwa Waziri wa Maji ukurasa wa 16, Ibara ya 34 naomba kunukuu; “Wizara imeendelea kuvitambua, kuviwekea mipaka na kuvitangaza vyanzo vya maji kuwa maeneo tengefu ili kuvilinda na kuvihifadhi kwa ajili ya kuzuia uharibifu na uchafuzi wa vyanzo hivyo.” Ombi langu ni kwamba hata vile vyanzo vya maji vya mamlaka mbalimbali vipatiwe hati miliki.

Mheshimiwa Naibu Spika, kasi ya uvunaji wa maji ya mvua bado iko chini kabisa, kwa masikitio makubwa sikuona kabisa msisitizo wa jambo hili kwenye hotuba. Ninaomba kujua Serikali ina mpango gani wa kunufaika na maji yanayotiririka hovyo na kupotelea baharini wakati wa mvua. Mfano, barabara ya Dar es Salaam - Dodoma eneo la Kibaigwa pande zote mbili maji yanatua na wakati mwingine yaliua, lakini hakuna juhudi za kuyatumia vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho ninakukumbusha mradi wa maji wa Nyumba ya Mungu - Mwanga, Same, Mombo, ni lini hasa utamalizika?

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja, naomba kuwasilisha.