Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu ujenzi wa Chuo cha Uhazili Tabora, naomba Serikali ikamilishe majengo hayo kwa hatua iliyobaki, kwani Chuo hicho kina historia kubwa katika Mkoa wa Tabora.
Mheshimiwa Naibu Spika, Walimu/Wakufunzi hawatoshi, pia usafiri wa Wanachuo hakuna na computer hazitoshi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Zahanati ya Chuo haina hadhi ya Chuo. Tunaomba Serikali ilione hilo ili kuwapa moyo wanafunzi hao. Tunaomba ukarabati wa vyoo ufanyike kwa vile vyote vya zamani. Kwani afya ya wanafunzi ni hatarini, pia itawaepusha na magonjwa hatari ya kipindupindu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba elimu itolewe kwa jamii ili watambue umuhimu na madhumuni ya TASAF III. Kabla fedha hazijatolewa, watendaji wote wapewe elimu kuhusu walengwa; Watendaji wa Kata/Vitongoji, Vijiji, Wenyeviti wote, Wajumbe wa maeneo husika. Wale wote walipewa nafasi, ambao siyo wahusika waondolewe kwenye orodha ya malipo hayo. Mikutano ya hadhara ni muhimu kwenye jamii kwa kushirikisha Wanasiasa.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.