Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza Serikali imeendelea kupunguza tatizo la maji nchini. Singida Mjini katika bajeti ya mwaka 2016/2017 tulipewa shilingi bilioni mbili mpaka sasa hivi fedha hizo hazijaja. Naiomba Serikali ituletee fedha hizo tuweze kukamilisha miradi ya maji iliyopo. Bajeti hiyo ya mwaka 2016/ 2017 Serikali pia iliahidi kutupatia fedha za fidia shilingi bilioni tatu kwa wananchi wa eneo la Irao - Kisaki waliopisha mradi wa maji mkubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, miradi ya vijiji kumi vya maji vinavyofadhiliwa na Benki ya Dunia, miradi hii imejengwa Singida Mjini bahati mbaya wananchi hawana maji mpaka sasa hivi. Naomba Serikali ije ifanye tathimini ya miradi hiyo na hatua za kinidhamu zichukuliwe kwa waliohusika kukwamisha miradi hiyo.