Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Capt. Abbas Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Fuoni

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. CAPT. ABBAS ALI MWINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka wa jana 2016 tulipata taarifa kuwa kuna fedha zilizopelekwa kwenda Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kutoka Serikali ya Muungano (Fedha hizo zinatoka Serikali ya India) kwa lengo la kufanya utatuzi wa kero za maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kweli kero hiyo inazidi kuwa kubwa na kutishia vibarua vyetu kama Wabunge. Je, fedha hizo kweli zilipelekwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Muungano ilipata mrejesho wowote juu ya suala hili? Serikali ya Muungano ina nini cha kusema kuhusiana na kadhia hii?

Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa kuwa Serikali ya India ina makusudio ya kuikopesha Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dola za Kimarekani 500 milioni na hatimaye Zanzibar kufaidika na fedha hizo, Zanzibar mgao wake ni kiasi gani kati ya hizo? Je, nini kinachokwamisha mkopo tajwa usitolewe mpaka sasa na hasa ukitilia maanani kuwa Ilani yetu ya Chama cha Mapinduzi inatuelekeza utatuzi wa kero hiyo?