Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niongelee kuhusu zuio la kulima vinyungu. Kilimo cha mabondeni (vinyungu) ni mkombozi wa wananchi wa Mafinga, Mufindi, Iringa na Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini. Hata hivyo, Serikali mmezuia kilimo cha vinyungu bila kufanya tathmini ya kina. Watendaji wa Serikali wameshindwa kutafsiri maagizo na kupanikisha (make panic) wananchi kwa kutishia kufyeka mazao yao, kuweka alama za ‘X’ na kuwapa notice ya siku tisini. Ndugu zangu lazima kuwe na tafsiri pana kuhusu mabondeni na vyanzo vya maji. Kuna maeneo ambayo kwa vigezo vyovyote wananchi hata wakilima haiathiri suala la mtiririko wa maji au vyanzo vya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kigezo cha mita sitini kisiwe uniform, kuna maeneo ingeweza kuwa mita kumi au ishirini. Nashauri very strongly tafsiri ya Sheria isipotoshwe. Kilimo cha mabondeni yapo maeneo hayahusiani na hayana connection na Mto Ruaha.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ziara ya Makamu wa Rais Mkoani Iringa kuhusiana na kuhuisha na kufufua vyanzo vya maji imetafsiriwa tofauti, sasa imekuwa ni vitisho, wananchi hawana amani. Nashauri na naomba suala hili lizingatie pia kuwa bado hatuna miundombinu ya kumwagilia, hivyo si kila eneo tuweke zuio la mita sitini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu Mafinga Mjini. Mji wa Mafinga pamoja na kuwa ni Halmashauri ya Mji bado kuna vijiji kumi na moja, naomba mipango ya Wizara izingatie kuwa pamoja na kuwa ni mji tuna maeneo ni vijiji, hivyo tusisahauliane katika mipango ya maji vijijini.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho, pamoja na kuwa suala la utumishi ni la TAMISEMI na Utumishi, ikama ya watumishi wa mamlaka ya maji ni wachache, Mhandisi wa Maji wa Halmashauri hana msaidizi, yuko peke yake. Naomba tuongezewe watumishi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.