Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niiombe Serikali iwasimamishe kazi wakandarasi wanaojenga Mradi wa Maji wa Nguluma Mlola kwa sababu wakandarasi hawa walitoa ahadi mbele ya Mheshimiwa Naibu Waziri kuwa Mradi wa Maji wa Ngulu ungekamilika tarehe 30 Aprili, 2017 lakini mpaka sasa hakuna hata dalili za kumaliza mradi ule pamoja na mradi wa Mlola. Miradi yote miwili imefikia asilimia 70 ya utekelezaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, niiombe Serikali yangu iwasimamishe au wapewe deadline ya kumaliza miradi yote hii miwili maana imekuwa kero kubwa kwa wananchi.