Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na pongezi zangu kwa Serikali kwa hatua kadhaa zinazochukuliwa kuboresha sekta ya maji na umwagiliaji nchini, nina mapendekezo yafuatayo:-

(i) Serikali iongeze bajeti kutoka bilioni mia sita hadi at least bilioni mia tisa iliyokuwepo.

(ii) Serikali iangalie uwezekano wa kuanzisha Wakala wa Maji kama ilivyo REA.

(iii) Tozo ya Sh.50/= kwa lita ya dizeli na petroli iongezwe kufikia Sh.100/= kwa lita.

(iv) Suala la majengo nchini kuwekewa miundombinu ya kuvuna maji ya mvua lisiwe la hiari bali liwe la kisheria ili kupata maji ya kutumia lakini pia kuzuia mafuriko nchini.

(v) Suala la sekta binafsi kujengewa mazingira ya kushiriki kikamilifu kwenye sekta ya maji hasa umwagiliaji, kupitia ubia wa Serikali na sekta binafsi (PPP)