Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Amb Dr. Diodorus Buberwa Kamala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. BALOZI. DKT. DIODORUS B. KAMALA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nibainishe kwamba naunga mkono hoja.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo la Nkenge kuna miradi ya maji ambayo tayari imepokea fedha zote za miradi husika ya maji lakini maji hayajapatikana. Miradi hiyo ni Mradi wa Maji wa Ruzinga, zimetumika zaidi ya shilingi milioni 400 na mradi wa maji wa Igurugati ambao umetumia zaidi ya shilingi milioni 300. Aidha, kuna miradi mingine ambayo nayo haitoi maji kama ilivyotarajiwa. Miradi hiyo ni miradi ya maji Kilimililite, Kakunyu, Kenyana na Kibeho.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Wizara ifuatilie kwa karibu miradi tajwa na hasa mradi wa Maji wa Ruzinga na Mradi wa Maji wa Igurugati ulio katika Kata ya Bugandika. Pia mradi wa Maji wa Kakunyu nao umeshindwa kutoa maji. Miradi yote tayari ilipokea fedha ya Benki ya Dunia lakini maji hayajapatikana.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitashukuru nikipata maelezo ya kina kuhusiana na miradi niliyobainisha.