Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kutoa mchango wangu katika Wizara hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, maji ni uhai, bila maji maisha hayawezi kwenda mbele. Naishauri Serikali iongeze tozo ambapo asilimia 70 ielekezwe vijijini na asilimia 30 iwe mijini, kwa kuwa kuna vijijini ndiyo kuna shida sana ya maji. Wanawake wa vijijini wamekuwa wakipata adha kubwa kwa ukosefu wa maji safi na salama. Wanashindwa hata kufanya shughuli za kiuchumi na maisha kuwa duni.

Mheshimiwa Naibu Spika, mamlaka nyingi za maji zinadaiwa bili za umeme kwa kushindwa kulipa na wao pia wanazidai taasisi nyingi za Serikali, hivyo kufanya wananchi wanaolipa bili za maji kukosa maji. Naishauri Serikali iweze kulipa madeni ya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Iringa yenye Majimbo mawili ya Kalenga na Isimani imekuwa na shida kubwa sana ya maji safi na salama wakati kuna vyanzo mbalimbali vya maji kama vile Mto Mtitu, Ruaha pamoja na chanzo kinachoitwa Ibofwe. Maombi mbalimbali ya fedha yametolewa, lakini utekelezaji wake haupo na inakatisha tamaa sana kwa wananchi ambao ni wapiga kura.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri Serikali iweze kutoa fedha ili maji yapatikane katika majimbo haya. Kuna maji ardhini ambapo pia, Serikali inaweza kuwekeza kwa kuchimba visima na maji yapatikane. Kwa hiyo, fedha ziwe zinatolewa kwenda kwenye Wizara hii ili waweze kufanya kazi ya kufumbua tatizo la maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri Serikali pia, ihimize uvunaji wa maji kwa kushauri kila anayejenga nyumba yenye bati kibali kitolewe tu kama ataweka na mfumo wa uvunaji maji, uchimbaji wa mabwawa na malambo hasa wakati wa masika ili kuvuna maji yatakayowasaidia wananchi; ni jambo la kutiliwa mkazo kwa Wizara hii. Naitaka Serikali/Mheshimiwa Waziri atakapohitimisha aniambie utekelezaji wa haya niliyoeleza ukoje?

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.