Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Asha Mshimba Jecha

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ASHA MSHIMBA JECHA: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.
Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Rais wetu, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa ufanyaji kazi ya utumbuaji majipu na nchi yetu kuwa ni mahali salama na wananchi wetu kukabiliana na maisha yao bila ya vikwazo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Makamu wa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu kwa kazi nzuri anazozifanya. Naamini kwa muda mfupi ujao maendeleo ya wananchi wetu yataboreka. Aidha, nawapongeza Mawaziri na Manaibu Mawaziri kwa utendaji kazi kwa kuwa karibu na wananchi, kubaini changamoto zinazowakabili na kuzipatia ufumbuzi wa haraka.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuchangia hoja hii ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Watanzania wameridhika na juhudi zinazoendelea kuchukuliwa katika kuwabaini wafanyakazi hewa na kuchukuliwa hatua zinazostahili. Kundi hili ni kubwa lina mtandao mrefu na usiri wa hali ya juu, lakini kila mmoja akichukua wajibu wake vita hii tutashinda.
Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa kazi wanazofanya kuangalia na kusimamia maadili ya Viongozi wa Umma. Nashauri Tume hii kuangalia na njia nyingine kwa kuwafikia wananchi ambao siyo Viongozi wa Umma katika utaratibu unaoeleweka, lakini wamekuwa viongozi katika mfumo usio rasmi.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kazi nzuri inayofanyika, nakubaliana na Wizara kuona ipo haja kufanya utafiti kwa waajiri na wadau mbalimbali ili kubaini changamoto ambazo zimekuwa zinalalamikiwa mfano, baadhi yao walipofuatilia Utumishi walijibiwa na mhusika kwamba bado haja-prove na kadhalika.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mfuko wa Kujitegemea (PTF) ni wa muda mrefu na umeweza kuwafikia watu wengi hasa wanawake. Tunashauri Mfuko huu utangazwe zaidi ili wananchi wetu waweze kufaidika nao.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja hii. Ahsante.