Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Mgeni Jadi Kadika

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. MGENI JADI KADIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia afya njema na kuniwezesha kuchangia Wizara ya Maji na Umwagiliaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, maji ni uhai wa binadamu, kila mtu anahitaji maji safi na salama ili awe na afya bora. Kila kiumbe kilicho ulimwenguni kinahitaji maji, maji ni uhai, maji ni kilimo, maji ni viwanda kila kitu kinahitaji maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi niko Kamati ya LAAC na nimetembelea miradi katika mikoa ya nchi yetu na kujionea hali halisi ya miradi ya maji na umwagiliaji. Miradi mingi imejengwa chini ya viwango, utakuta mradi ni mkubwa na unagharimu fedha nyingi lakini wananchi hawapati maji. Aidha, pipe ni nyembamba haiwezi kusambaza maji kwa vijiji vyote, kwa mfano vijiji sita watapata vijiji viwili, hili ni tatizo. Ikumbukwe hii ni Wizara kubwa na yenye mahitaji makubwa. Naomba bajeti ya maji iongezewe fedha ni ndogo.

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi wa umwagiliaji Inalia. Mradi huu uko katika Manispaa ya Tabora, ni mkubwa na umegharimu fedha nyingi, jumla ya Sh.246,536,679, hizi fedha ni nyingi. La kusikitisha, mradi huu umekamilika zaidi ya miaka saba sasa lakini haujafanya kazi kwa sababu wamiliki wa mashamba haya mpaka leo hawajalipwa fidia ya mashamba yao na kupelekea mgogoro mkubwa baina ya Halmashauri na wenye mashamba. Mradi una ukubwa wa ekari 110 na wale wananchi waliopewa wameukataa kutokana na mgogoro huo. Je, Serikali ni lini watawalipa wananchi hao fidia ili mashamba hayo yaweze kuendelezwa? Namwomba Waziri aende akatatue mgogoro kwa sababu waathirika wakubwa ni wanawake kuhusu matatizo ya maji, wanapoteza muda mrefu kutafuta maji na wengine ndoa zao kuvunjika.

Mheshimiwa Naibu Spika, vyoo mashuleni kukosa maji ni tatizo kubwa lakini ni tatizo kubwa zaidi kwa mtoto wa kike pale anapokuwa kwenye siku zake za hedhi inambidi akae nyumbani na kusababisha kukosa masomo. Je, Serikali ina makakati gani kuhakikisha tatizo la maji linaondoka?

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya mchango wangu huu, naomba kuwasilisha.