Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. ELIAS J. KWANDIKWA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nianze kwa kuunga mkono hoja.

Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru Mheshimiwa Waziri kwa hotuba nzuri, nashukuru Serikali kwa kuendelea kutuboreshea huduma za maji katika maeneo yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, maji toka Ziwa Viktoria. Utakumbuka maji ya Ziwa Viktoria yamefika katika Mji wa Kahama na yanapelekwa Nzega na Tabora lakini hayakusambazwa Jimbo la Ushetu ambalo liko Wilayani Kahama. Jimbo la Ushetu linashikilia 57% ya eneo la Kahama, wananchi wa Ushetu wanahisi kutengwa kwani maji haya yanawazunguka. Pia maji yanayotoka Mto Malagarasi watayatazama tu majirani zao wa Halmashauri ya Ushetu. Kwa kuwa tulifanya kikao na Mheshimiwa Naibu Waziri na wataalam wa Wizara tarehe 3/5/2017 na kugundua kuwa tulikuwa tumeahidiwa kuunganishwa mwaka 2014, naiomba Wizara ianze tena mchakato wa kutuletea maji katika Halmashauri ya Ushetu toka mradi wa Ziwa Viktoria.

Mheshimiwa Naibu Spika, umwagiliaji. Naiomba Wizara iongeze juhudi za utafiti ili tuweze kutafiti maeneo ambayo tunaweza kutengeneza mabwawa ili yasaidie kwenye kilimo cha umwagiliaji. Ushetu tunayo maeneo yenye rutuba na ambayo yanafaa kuweka skimu za umwagiliaji. Maeneo hayo ni kwenye Kata za Uyogo, Idahina na Sabasabini. Wizara itusaidie utaalam huo na kuelekeza nguvu ili tuweze kuchangia malighafi za viwanda vyetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, miradi mipya. Utaratibu wa kutekeleza miradi mipya iliyotengewa fedha haujaeleweka kwani Halmashauri zinasubiri fedha ili kuweka kandarasi. Tunaomba zoezi lisimamiwe vema na sisi Wabunge tushirikishwe ili miradi ianze kwa wakati na certificate zitoke ili miradi ikamilishwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.