Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Yosepher Ferdinand Komba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. YOSEPHER F. KOMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, fedha itengwe kwa ajili ya kutoa elimu kwa wananchi hasa majumbani (house hold water treatment). Hii itasaidia kupunguza maradhi yanayotokana na maji kuchafuka.

Mheshimiwa Naibu Spika, uchakavu wa miundombinu. Wilaya ya Muheza ni moja kati ya Wilaya ambazo zina miundombinu chakavu sana. Je, Wizara imeandaa utaratibu gani ili kuboresha miundombinu hii kwa kuwa kuna miradi mingi inaanzishwa lakini kwa uchakavu huu haiwezi fanikiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, treatment plant. Mji wa Korogwe unahitaji chujio na treatment plant yenye gharama ya shilingi bilioni sits. Wafadhili toka Australia wameonesha utayari wa kutoa mkopo wa riba nafuu kwa Mji wa Korogwe.

Je, Serikali iko tayari kusaidia Mji wa Korogwe kupata mkopo huo?

Mheshimiwa Naibu Spika, uvunaji wa maji. Wizara imeandaa utaratibu gani wa kusimamia Halmashauri ambazo hazijatengeneza Sheria Ndogo katika Halmashauri zao ili kila anayejenga nyumba yenye bati (shule na hospitali) aweke mifumo ya uvunaji maji?

Mheshimiwa Naibu Spika, nawasilisha.