Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo la maji ni kubwa sana katika nchi yetu, tunapaswa kuisaidia jamii yetu kwa kupanga namna nzuri ya kutatua tatizo hili. Kuundwa kwa Wakala wa Maji Vijijini kutatuongezea sh.50/= + Sh.50/= tutapata Sh.100/= ili kuweza kutatua tatizo hili, kama REA.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika miradi inayoendelea kutekelezwa, tuna tatizo kubwa la fedha kwa Wakandarasi ambao wanapoleta certificates zao hawalipwi kwa muda unaotakiwa. Mfano, Mradi wa maji wa Haydom umeshindwa kulipwa na vyeti vyao vipo Ofisini kwa Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia kuna wakati mwingine hulipwa nusu ya walichokidai, hebu Mheshimiwa Waziri atusaidie mradi huu uishe kwa kuwapatia fedha Miradi ya Haydom, Arry, Ampa, Bashau. Mheshimiwa Naibu Waziri alitembelea Bwawa la Dongobesh, naomba ahadi yake aliyoitoa Haydom na Dongobesh itekelezwe kwa kuleta fedha kwa haraka.

Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kutembelea Wilaya ya Jimbo langu. Ombi langu ni kuwatimizia wananchi huduma hii ya maji. Maji mengi wakati huu wa mvua nyingi hupotea. Naomba tusaidiwe na wataalam ili tupange kuyazuia maji kwa kujenga mabwawa ya kumwagilia maana kilimo peke yake chenye uhakika ni kilimo cha kumwagilia.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunapanga bajeti lakini fedha hazitoki kulingana na tulivyopanga. Hivyo, ni vema kupeleka fedha kwa wakati ili kuona matokeo ya haraka. Narudia ili ukumbuke, “fedha za miradi ya Dongobesh – Bwawa; Haydom – Mradi wa Maji; na Arry – Tumati, Mradi wa Maji.”