Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Martin Alexander Mtonda Msuha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. MARTIN M. MSUHA: Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue nafasi hii kuungana na Waheshimiwa Wabunge walioipongeza Wizara kwa kazi nzuri inayoendelea kutekelezwa kupitia miradi mbalimbali ya maji. Kama Mjumbe wa Kamati ya LAAC nilifanikiwa kutembelea miradi kadhaa ya maji na umwagiliaji katika Mikoa, Wilaya za Lindi Manispaa, Nachingwea, Singida Manispaa pamoja na Tabora Manispaa. Kwa ujumla wake kati ya miradi yote tuliyotembelea haikutekelezwa kwa kiwango cha kuridhisha kabisa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri Wizara kuunda team maalum kufanya tathmini ya miradi yote ya maji na umwagiliaji iliyotekelezwa kuanzia mwaka 2012/2013. Hili ni muhimu sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivi karibuni wakati wa Mbio za Mwenge Wilayani Mbinga kulikuwa pia na uzinduzi wa mradi wa maji katika Kata ya Mkako Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga. Mradi huu ulikataliwa na wananchi kwa sababu umetekelezwa chini ya kiwango kwani mabomba yameunganishwa kwa moto badala ya connectors. Naomba Wizara ipeleke wataalam wake ili kubaini ubadhirifu huu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitaleta malalamiko haya rasmi kwa maandishi ofisini kwa Mheshimiwa Waziri wa Maji kwa hatua zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naiomba Wizara ikamilishe visima vinne katika program ya visima 10 katika kila Jimbo. Visima hivyo vinne vipo katika Kata ya Litumbandyosi. Ushauri wa ujumla ni kwamba yapo maeneo ambayo kama wananchi watashirikishwa kikamilifu kwenye miradi ya maji, itapunguza sana gharama za miradi husika. Mfano, Wilayani kwetu Mbinga kuna vyanzo vingi vya maji vya gravity. Wananchi wapo tayari kujitolea kufanya kazi kama uchimbaji mitaro na kazi nyingine za kutumia nguvu.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Wizara ituletee wataalam Wilayani Mbinga ili kutengeneza miradi shirikishi ya maji katika miji, Kata ya Maguu, Ruanda, Matiri, Nyoni, Litembo, Mikalanga, Ilela, Kambarage, Mkumbi, pamoja na Kindimba Juu. Hii inaweza kuwa model kwa maeneo mengine katika nchi hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya mchango huu, naunga mkono hoja.