Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Mahmoud Hassan Mgimwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. MAHMOUD H. MGIMWA: Mheshimiwa Naibu Spika, pongezi kwa Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri kwa kazi nzuri wanayoifanya katika Wizara hii. Naungana na Kamati yangu ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu kuongeza tozo kwenye mafuta ili kuboresha Mfuko wa Maji. Ni vyema Serikali ikakubaliana na hoja za Waheshimiwa Wabunge kuhusu kuongeza tozo kwenye Wizara hii ili kuongeza pesa ambazo zitapelekwa kwenye Majimbo mbalimbali kutatua kero kubwa ya maji ambayo inawaumiza akinamama wengi waliopo vijijini.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo langu kuna mradi mkubwa wa Kihata ambao tumeuombea mara nyingi hapo Wizara ya Maji. Kwa masikitiko makubwa, mpaka leo hatujajibiwa. Ni vyema Serikali ikawa inatoa support kwenye taasisi zinazojitolea kuwekeza katika Sekta ya Maji. Katika Jimbo la Mufindi Kaskazini kuna NGO inaitwa RDO, imewekeza kwa kiasi kikubwa katika Sekta hii ya Maji, lakini Serikali imekuwa haitoi support ya aina yoyote. Namwomba sana Mheshimiwa Waziri tukutane na NGO hii ili Serikali iweze kuwekeza pia. Ni vyema sasa Serikali ikasimamia na kujua kwa nini misaada ya World Bank haijakamilika mpaka leo; na pesa zinapotea bure? Ni vyema Mheshimiwa Waziri anapohitimisha atuambie ni hatua zipi zitachukuliwa na Serikali kwenye hii miradi.

Mheshimiwa Naibu Spika, bwawa la mto Liandimbela mpaka leo imekuwa hadithi. Mwaka 2014 Mheshimiwa Pinda Waziri Mkuu Mstaafu aliahidi shilingi milioni 295 kwa ajili ya kuendeleza bwawa la umwagiliaji wa Nundwe. Mpaka leo maji ni tatizo, lakini hakuna uwiano wa kupeleka fedha za maendeleo katika Majimbo yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.