Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Kigoma Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. KABWE Z. R. ZITTO: Mheshimiwa Naibu Spika, hivi karibuni kumetokea kero kubwa ya maji kwa wananchi wengi wa mijini kufuatia madeni ya umeme. Manispaa ya Kigoma-Ujiji imehusika moja kwa moja na suala hili kufuatia deni la shilingi bilioni 1.2. Hivi sasa kuna Mradi mkubwa wa Maji Kigoma. Naishauri Serikali kwamba mradi huu tutumie umeme wa jua kuendeshea mitambo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri mradi ufanyiwe marekebisho hayo, kwani kutumia umeme wa TANESCO siyo endelevu, kwani gharama ni kubwa. Kuna wafadhili wengi sana wanaowekeza kwenye nishati jadidifu, tuzungumze nao ili miradi inayoendelea sasa itumie nishati mbadala. Suala hili niliongea mwaka 2016/2017. Naomba Serikali litazameni hili, undeni kikosi kazi cha kulitazama hili la umeme wa jua kuendesha miradi ya maji mipya.

Mheshimiwa Naibu Spika, miradi mingi ya maji inayoendelea au kupangwa, inahitaji inputs ambazo nyingi zinaagizwa kutoka nje. Serikali inataka kuendeleza viwanda, ni vema kufungamanisha miradi hii na dira ya maendeleo ya viwanda. Tutazame orodha ya miradi na vituo vinavyotakiwa vikiwemo mabomba, madawa na kadhalika. Kisha tuone namna ya kuhamasisha sekta binafsi kujenga viwanda vya kuzalisha vifaa vinavyotakiwa kwenye miradi hii, hata ikibidi kuwapa guarantee sekta binafsi, tufanye hivi tuache kufanya miradi bila kutazama picha kubwa. Miradi.

mikubwa ya maji yaweza kuchochea maendeleo makubwa ya viwanda, kuongeza ajira na kutokomeza umaskini. Tusifanye kazi kwa kutazama eneo moja, bali tuwe multidisciplinary.