Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Peter Joseph Serukamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ya kwangu ni machache, moja, Jimbo langu la Kigoma Kaskazini tuna vijiji 46, katika vijiji 46 vijiji ambavyo maji yanatoka ni vijiji 14. Ningemuomba sana Mheshimiwa Waziri atusaidie na sisi watu wa Kigoma Kaskazini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kigoma na mikoa mingine, niombe sana Mheshimiwa Waziri umefika wakati tuyatumie maji ya Lake Tanganyika kwa ajili ya kupeleka maji Kigoma na all the way mpaka Tabora. Kwa sababu kutumia mito, mito inakauka. Ukienda leo uangalie Malagarasi ng’ombe walioingia mle na hali ya Malagarasi tukitumia kama itasaidia kwa wengine ni nguvu sana.

Mimi niombe Waziri, imefika wakati tufanye maamuzi ya kuchukua maji ya Lake Tanganyika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bajeti ya Wizara ya Maji. Nimewasikiliza sana wenzangu hapa ndani, bajeti haitoshi. Kwangu bajeti hii inatosha, nitasema kwa sababu gani. Watu wote humu ndani naomba tuchukue Kitabu cha Nne, ukichukua Kitabu cha Nne nenda kila mkoa kwenye sub vote 3280 kuna Rural Water Supply, kila mkoa kuna fedha, lakini hizo haziko kwenye Wizara ya Maji. Naweza nikataja baadhi ya mikoa, Ruvuma wana shilingi bilioni nane, Kilimanjaro wana shilingi bilioni nne, Kagera wana shilingi bilioni nne, Tanga wana shilingi bilioni mbili, Kigoma wana shilingi bilioni tatu. Ukizijumlisha zote hizi na ukaja na za bajeti, bajeti ya maji inatosha. Sasa ambalo nataka Mheshimiwa Waziri wa Fedha atupe commitment, fedha hizi zitoke zote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli mwaka wa jana ilikuwa bilioni 900, zimekwenda asilimia 19; na Waheshimiwa Wabunge tusipende ma-figure makubwa sisi tujaribu kuhangaika fedha tunazopitisha ziende. Haya ndiyo maswali ya sisi kujiuliza, kwa sababu kama tunakaa hapa miezi mitatu tunapitisha bajeti halafu zinakwenda asilimia 19 halafu mwaka ujao sisi tunasema hapana bajeti haitoshi iongezeke. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi mbona hatuongelei asilimia 80 ambazo hazijaenda? Kwa hiyo mimi nasema kama ni bilioni mia sita ikitokea zikaenda zote mwaka huu maana yake ni kwamba tutakuwa tumefanya asilimia 75 ya yale ambayo tungefanya mwaka jana, asilimia 75 ni pakubwa mno. Kwa hiyo,…

T A A R I F A . . .

MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, huyu ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti, ananishangaza kidogo. Mimi sijaongelea habari ya tozo hapa, naongelea habari ya bajeti, anataka kuniambia shilingi bilioni 900 za mwaka jana zote zilikuwa za tozo, unataka watu wote hapa tuamini kwamba shilingi bilioni 900 zilikuwa za tozo? Sijaongelea jambo hilo, ninachoongea mimi, naongelea bajeti ya Serikali…

T A A R I F A . . .

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niwakumbushe Waheshimiwa Wabunge nilichoongea mimi hapa hakuna ninayempinga hata mmoja. Ninachosema, nataka kuwaonesha Waheshimiwa Wabunge kwamba kwenye fedha zinazokwenda mikoani kwetu nyingine ziko kwa ma-RAS, hakuna anayesema mwaka jana, mwaka juzi zilikuwepo. Kwa hiyo, tunapoongelea bajeti ya maji ya mwaka jana ilikuwa ni shilingi bilioni 900 plus hizo za mikoani na ninavyosema mwaka huu ni shilingi bilioni 600 plus zilizo kwa RAS na fedha za RAS hazipiti Kamati ya Kilimo, kuna Kamati ya TAMISEMI; Kamati ya TAMISEMI Ndiyo inaangalia fedha zote za TAMISEMI.

Mheshimiwa Mwenyekiti, TAMISEMI kule kuna fedha za elimu, kuna fedha za maji, kuna fedha za kilimo, kuna fedha za kila kitu, kuna fedha za afya. Unapotaka kuongelea maji in Tanzania huwezi kusema zile unaziondoa, na zenyewe ni sehemu ya kutatua tatizo la maji kwenye mikoa yetu. Argument yangu ni fedha ziende, kwamba Waheshimiwa Wabunge tusikae hapa eti Mheshimiwa Waziri akija ameweka 1.4 trillion tusimame tumpongeze halafu mwaka unaofuata zimeenda shilingi bilioni 200, tunapata nini? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunachosema hapa, fedha iliyopangwa iende, ikienda nina hakika hali ya maji kwenye nchi yetu itabadilika. Lakini tukianza kunyoosheana vidole, yule amepangiwa nyingi mimi chache haina maana. Sisi twende kwenye plan yetu, zimetoka shilingi bilioni 600 tuiombe Serikali kwa mara ya kwanza waweke commitment kwamba zote shilingi bilioni 600 zitakwenda; na baada ya shilingi bilioni 600 ninazoongelea kuna nyingine kwenye mikoa yetu. kwa hiyo unaweza ukakuta tunaongelea bajeti ya maji in totality zaidi ya shilingi bilioni 800 si fedha ndogo.

heshimiwa Mwenyekiti, mimi nilitaka kusema kwamba jambo la msingi tuhangaike fedha zetu ziende, na hii itatusaidia sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho ni suala la DAWASCO na DAWASA. Umefika wakati kwa spirit ile ile ya kubana matumizi, nikuombe vyombo hivi viunganishwe ili viweze kubana matumizi viweze kufanya kazi nzuri katika Mji wa Dar es Salaam...

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.