Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Catherine Nyakao Ruge

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. CATHERINE N. RUGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakusukuru kwa kunipa fursa ya kuchangia kwa mara ya kwanza kabisa katika Bunge lako hili Tukufu. Napenda kuchukua nafasi hii kutoa pole kwa Watanzania, kwa familia, kwa Wabunge, ndugu jamaa marafiki na bila kusahau Mbunge wa Arusha Mjini Mheshimiwa Godbless Lema kwa msiba uliolikumba Taifa hili siku chake zilizopita, Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi, Amina. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo naomba niungane na Waheshimiwa Wabunge wenzangu waliotangulia kuchangia, kwamba Serikali iweze kuongeza bajeti ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa kuzingatia umuhimu wa maji katika maisha yetu ya kila siku. Serikali inaweza ika-pull resource kutoka kwenye sekta nyingine na tuweze kuipa kipaumbe Wizara hii ya Maji ambayo ni muhimu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nisikitike kusema kwamba pamoja na kuwa na vyanzo vingi vya maji katika nchi yetu, kwa maana ya maziwa, mito, mabwawa na mabonde mbalimbalil changamoto ya maji imekuwa ni ya muda mrefu. Tangu mimi nimezaliwa mpaka sasa hivi bado namwona mama yangu na wanawake wengine wa Kitanzania wakiwa wanabeba ndoo kichwani ikiwa ni zaidi ya miaka 30. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto ya maji inawaathiri pia wanafunzi wa kike kwa sababu mashuleni hakuna maji, hasa sehemu za vijijini. Hii inafanya watoto wa kike wakiwa katika hedhi washindwe kuhudhuria masomo kati ya siku tatu mpaka tano, jambo ambalo hupunguza ufaulu wa masomo kwa sababu ukichukua siku tano katika mwaka ina maana wanakosa masomo takriban siku 60 kwa mwaka. Kwa hiyo, niiombe Serikali iangalie jinsi gani inaweza kuboresha miundombinu ya maji katika shule zetu ili tuweze kuwasaidia watoto wa kike waweze kufaulu vizuri kwa kuweza kuhudhuria masomo yao kila siku. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie kuhusu miundombinu ya maji katika jimbo la Serengeti ninalotoka mimi. Ukiangalia bajeti hii ya mwaka 2017/2018 ni shilingi milioni 858 tu zilizotengwa katika jimbo la Serengeti. Kuna changamoto nyingi sana ambazo zinalikabili shirika la maji safi na taka la MUGUWASA ambalo lina wakazi 47,000 kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2012.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto ni nyingi ikiwa mojawapo pump ni moja ambayo haikidhi mahitaji, lakini pia kuna tenki moja tu ambalo halitoshelezi kwa wananchi wa Mugumu Mjini, mji ambao ambao unaundwa na kata saba zilizoko pale. Kwa hiyo, niiombe Serikali iweze kuongeza bajeti katika eneo hili ili kuweza kuboresha miundombinu ya maji katika mji wa Mugumu kwa sababu miundombinu ni ya zamani sana na imechoka, lakini pia gharama za uendeshaji ni kubwa sana za Mamlaka ya Maji ya Mugumu Mjini kwa sababu makusanyo ya mwezi ni shilingi milioni saba lakini wanalipa ankara za umeme shilingi milioni 16.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii inaonesha kabisa mamlaka ya maji Mugumu Mjini inajiendesha kwa hasara. Kwa hiyo, tuangalie nishati mbadala ambayo inaweza kuendesha ile pump ya Manchira ili tuweze kupunguza gharama za uendeshaji, lakini pia tupunguze gharama kwa watumiaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto nyingine ambayo inaikumba MUGUWASA ni kwamba kuna upungugu wa mita kwa wateja. Kati ya wateja 1,536 ni wateja 509 tu ambao wameunganishiwa mita za maji. Kwa maana hiyo hii inaikosesaha mapato Muguwasa. Kwa hiyo, niiombe Serikali iangalie jinsi ya kuisaidia MUGUWASA kuweza kusambaza mita ili wateja wote waweze kupata mita na hivyo waweze kuchangia mapato ya MUGUWASA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika bajeti hiiā€¦

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga hoja Kambi Rasmi ya Upinzani.