Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba nianze kwa kuunga mkono hoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hapo na mimi niungane na wazungumzaji wote wanaozungumzia habari ya Wizara kuongezewa fedha. Sambamba na hilo, wenzetu wa sheria wana usemi wao wanaosema; “Justice must not only be done, but must be seen to be done” ikiwa na tafsiri gani? Leo hii tunapozungumzia habari ya Wizara na fedha, inawezekana mwaka wa jana bajeti ile ilikuwa kubwa, safari hii tunapotamani tena kuwa na bajeti kubwa, tatizo ninaloliona mimi si ukubwa wa bajeti, ni utekelezaji kwa maana ya fedha zifike kwa walengwa, hilo ndilo tatizo ninaloliona. Kwa hiyo, kwa tafsiri hiyo, kama tuliweza kutekeleza kwa asilimia 19 vipi kama fedha ikienda hata kwa nusu ya bajeti ikiwafikia walengwa? Kila mmoja hapa atapunguza kupiga kelele, mimi ndiyo naliangalia kwa sura hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikija kwenye mji wangu wa Mpanda nafahamu miundombinu ya maji katika mji ule imechakaa, sehemu kubwa ni mabomba ya chuma, nilikuwa naomba Wizara iliangalie suala hilo. Leo hii tuna maeneo ya Makanyagio, Majengo, Majengo A na B, zote hizo kwa kweli hazifikiwi na maji kutokana na uchakavu wa miundombinu. Nafahamu tunalo Bwawa la Milala, tuna changamoto ya uwepo wa viboko. Bwawa lile lilikuwa na uwezo mkubwa wa ku-supply maji, niendelee kuomba wahusika waliangalie hilo, ili kukidhi suala hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nafahamu tunao Mradi wa Ikorongo, ule mradi peke yake haukidhi mahitaji ya maji kwa Manispaa ya Mpanda. Tuna maeneo ya Mwamkuru, maeneo haya naendelea kuyaombea visima. Kuna wakazi wengi, lakini ukiangalia maeneo yale mpaka leo hii suala la visima ni tatizo. Eneo hilo hilo la Mwamkuru tuna skimu ya umwagiliaji ya Mwamkuru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo nasikitika kusema tunakwenda mwaka wa saba skimu ile haijafanya kazi. Ni tatizo, kwa hiyo nilikuwa naomba Waziri atakapokuja hapa aniambie tunafanya nini katika eneo hili, na ukizingatia watu wale kwa kupitia skimu za kwao wenyewe wamekuwa wakizalisha chakula cha kutosha. Leo hii mwarobaini ilikuwa ni skimu hii ambayo ingeweza kusaidia eneo lile likafunguka na chakula kikapatikana cha kutosha. Naomba niambiwe kwa nini tunakwenda mwaka was aba sasa hivi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuyasema yote hayo, nilikuwa naomba pia nielezee uelekeo pekee wa kusaidia mji wetu wa Mpanda kwa kweli ni kuyatoa maji kutoka Ziwa Tanganyika. Najua hii tunapozungumzia habari ya Ikorongo ni chanzo cha muda mfupi, tutapoteza muda mwingi kuzungumzia chanzo ambacho hatuna uhakika wakati chanzo cha uhakika kipo. Niombe na kwa wakati tofauti nimeshaongea na Mheshimiwa Naibu Waziri, aliangalie hili lianze kuingia kwenye mpango wa kuyatoa maji Ziwa Tanganyika na kuyaleta katika maeneo hayo, hata mikoa mingine ya jirani. Kwa kweli pale kilometa ni chache. Kilometa za kutoka Karema kuja Mpanda Mjini hazizidi mia au ni mia na kidogo, ni umbali mdogo huo. Nilikuwa naliomba hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naendelea kusisitiza, eneo la umwagiliaji ni ufumbuzi wa kutosha katika nchi hii. Mimi niombe, kwa maana ya umwagiliaji, leo hii tusilalamike; niliwahi kusema hapo mwanzo kwamba nchi hii tumebahatika kuwa na vyanzo vingi. Sizungumzii habari ya Bahari ya Hindi, nchi nyingine zinahangaika ku-treat maji ya bahari, sisi hatujafika huko…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)