Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Hon. Abdulaziz Mohamed Abood

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji

MHE. ABDUL-AZIZ M. ABOOD: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kunipa nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nipende kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kazi nzuri anayoendelea kuifanya ya kutekeleza ahadi za maji katika Jimbo letu la Morogoro Mjini. Tunamshukuru alituahidi atatupa mradi wa maji na kweli sasa tumepata mradi wa maji, naishukuru sana Serikali, ila ninachoomba kwa Mheshimiwa Waziri tuharakishe huu mradi wa maji ambao tulimepewa na Wafaransa ili kuondoa kero hii ya maji, na hasa wakazi wa Morogoro wanazidi kuongezeka wakiwemo Wabunge wengine humu wakihamia Morogoro.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tuna eneo la uwekezaji ambalo linahitaji maji mengi kwa ajili ya kuwekeza kwenye viwanda na wawekezaji wengi wakija kitu cha kwanza wanachouliza ni maji. Kwa hiyo, tunaomba Wizara iharakishe kazi hii ya mradi huu wa maji ili tuweze kupata maji kwa wakati. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Morogoro bado kuna tatizo la maji. Huu mradi ni mradi wa muda mrefu lakini sasa hivi bado tuna tatizo la maji. Bwawa la Mindu limejaa lakini miundombinu inayokwenda na kusambaza katika maneo mbalimbali ya Morogoro bado ni tatizo. Kwa hiyo, naomba Wizara iliangalie hilo ili kuongezea bajeti upande wa Morogoro kwa ajili ya kuweza kutengeneza miundombinu mipya ambapo maeneo mengi kuna miundombinu chakavu; na hasa maeneo ya Kihonda, Tungi, Lukobe, Mkundi na Kiyegeya. Cha kushangaza zaidi wananchi wa Mindu ambao wanalilinda lile bwawa la maji kwao hakuna maji wala miundombinu ya maji, kwa hiyo, naomba Wizara waliangalie hilo ili tuweze kuondoa kero hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna miradi ya World Bank ambayo wananchi wamechangia. Sasa kuna tatizo ambalo Mheshimiwa Waziri naomba hili mlifanyie kazi, kuna kata mbili kata ya Bigwa na Kingolowila, kuna mitaa minne ambayo wananchi wamechangia mradi huo lakini mradi huo unataka kuchukuliwa na kupewa MORUWASA. Ila wananchi sasa wanadai wanasema miradi wameshachangia wao wanahitaji wao wenyewe waendeshe hiyo miradi ya maji kwa kutumia vikundi vyao vya ushirika. Tatizo linalokuja ni kusema kuwa sheria hairuhusu. Mimi nadhani wakati wananchi walipokuwa wakichangia ilitakiwa waambiwe kwamba mradi huu hamtoweza kuendesha wenyewe. Sasa hivi kuna mgogoro mkubwa sana katika maeneo haya. Kwa hiyo, namuomba Mheshimiwa Waziri, elimu ya kutosha inatakiwa kwa wananchi ili kuepukana na tatizo hili la kudai kuendesha mradi huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi huu wamepewa MORUWASA na bei wanayowapangia sasa hivi ni kubwa, kwa hiyo, hawakubaliani nao na mradi umesimama na wananchi bado wanaendelea kukosa maji. Tunaomba hili tatizo lifanyiwe kazi ili tuweze kulimaliza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna tatizo lingine kubwa bado linaendelea na hasa tunategemea kupata mradi mkubwa wa maji, Mjini Morogoro. Tatizo ni bili za maji wananchi wanalipa maji ambayo kwa mwezi mzima au miwili hajapata lakini anapata bili ametumia maji, ni kutokana na mita zenyewe…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.