Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichukue nafasi hii kumpongeza Rais, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli na timu yake mahiri ya Mawaziri kwa kazi nzuri wanayofanya na hasa ya kutumbua majipu na kuinua uchumi wa nchi yetu ya Tanzania.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuondoa umaskini kupitia TASAF; pamoja na mafanikio makubwa yatokanayo na mpango wa kunusuru kaya maskini, TASAF, kuna changamoto nyingi ambazo zinatakiwa kushughulikiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, natoa rai kwa Serikali kuhakikisha changamoto mbalimbali zinazotokana na utekelezaji zinatatuliwa ili kuhakikisha fedha hizi zinakidhi malengo. Serikali ihakikishe TASAF imetimiza malengo ya kuondoa umaskini. Napendekeza mpango huu wa TASAF uboreshwe hasa usimamizi wa kutambua kaya maskini. Pia napendekeza hasa katika maeneo ya vijijini fedha ya TASAF itumike kuboresha huduma za kijamii ili hiyo pesa kidogo ifanye kazi pana zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu Utawala Bora; pamoja na muundo mzuri wa Serikali na taasisi zake, kuna changamoto ya nafasi nyingi za Uongozi kuwa na Makaimu kwa muda mrefu. Pia kuna Mashirika mengi ya Umma yanaendeshwa bila Bodi za Wakurugenzi kwa kipindi kirefu. Hii inapelekea Idara na Mashirika hayo kutoendeshwa vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, natoa rai kwa Serikali kuboresha uteuzi wa Bodi za Wakurugenzi, kuzingatia taaluma na uwezo badala ya uwakilishi wa Idara za Serikali. Msajili wa Hazina (TR) ahusike kikamilifu katika zoezi la kuteua Wakurugenzi wa Bodi. Pia Serikali izingatie uwezo na taaluma katika kuteua Wakuu wa Idara wakiwemo Wakurugenzi wa Halmashauri na Viongozi wengine.
Mheshimiwa Naibu Spika, natoa rai kwa Serikali kutowavumilia Viongozi na Watumishi wenye tuhuma za ubadhirifu na uadilifu wa mashaka, badala ya kuwahamisha au kubadilisha kituo waondolewe kwenye Utumishi wa Serikali na Taasisi zake.