Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa nafasi uliyonipa. Kwanza naomba nimpongeze Waziri na Naibu Waziri wa Wizara hii nyeti kwa manufaa ya Watanzania kwa kazi kubwa ambayo wanaifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimepitia hotuba hii, kwa kweli inatoa mwelekeo mzuri wa kutufikisha mahali ambapo tutakuwa kwanza tuna chakula cha kutosha, lakini pia tutaendeleza uchumi wa viwanda ambapo sehemu kubwa itategemea kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesikiliza Waheshimiwa Wabunge wengi wanavyochangia na wameishauri Serikali kwamba ni vizuri tuwe na mkakati wa kutosha wa kuinua kilimo cha umwagiliaji. Ni kweli nakubaliana nalo na ni kweli kwamba asilimia zaidi 75 ya kilimo chetu tunategemea mvua na kilimo cha mvua kwa kweli siyo endelevu, kama mvua hakuna maana yake hakuna kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kwa vyovyote vile lazima tuweke mkakati na ndiyo maana tayari tumeanzisha Tume ya Umwagiliaji ambayo ndiyo itakayosimamia eneo hili la umwagiliaji. Tumeona tuwe na Tume ili wawe na nguvu zaidi kuliko kufanya kama idara ya Serikali. Kwa hiyo, Tume tunayo na sasa hivi wanaandaa mpango kabambe wa umwagiliaji katika Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema kwenye bajeti yangu kwamba tuna hekta 29,000,000 zinazofaa kwa kilimo cha umwagiliaji. Bahati nzuri tumepata msaada kutoka shirika la JICA ambalo limetufadhili kuandaa mpango ule, sasa hivi tunafanya manunuzi ya kupata Mhandisi Mshauri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa muda mrefu katika kuendeleza sekta ya kilimo tumekuwa na miradi midogo midogo ya kusaidia wakulima wadogo wadogo, kila Halmashauri imekuwa na miradi lakini kwa sehemu kubwa miradi hii haijawa endelevu. Kwa hiyo, sasa tunataka tufanye mkakati wa kuhakikisha kwamba miradi hii ya umwagiliaji ambayo iko kwenye Halmashauri zetu inakuwa endelevu kwa kuipa nguvu kupitia hii Tume ya Umwagiliaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kazi kubwa na ya muhimu kwanza maji kama ambavyo wanavyosema ni muhimu kwa binadamu lakini ni muhimu kwa mifugo yetu na ni muhimu kwa kilimo. Kwa hiyo, tutajenga mabwawa na mabwawa haya haya ndiyo tutakayoyatumia tupate maji
ya umwagiliaji ili tuweze kuinua kilimo chetu na tuwe na uhakika wa chakula.

Mheshimiwa Mwenyekiti,Kwa hiyo, hii ndiyo kazi kubwa ambayo tunakwenda kufanya, hatutaweza kuendeleza kilimo kwa kutegemea mvua. Kwa hali ya tabia ya nchi inavyoonekana sasa mvua imekuwa inapungua kila mwaka kwa hiyo tukitegemea mvua kilimo chetu kitakuwa si endelevu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.