Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kupata nafasi hii ya kuchangia hotuba ya Wizara ya Kilimo. Kilimo kwangu mimi ni Wizara mama kwani wazazi wangu walionipa maisha haya wamenilea na kunisomesha kwa kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, viongozi wote wa Tanzania kuanzia vitongoji hadi Taifa na Watanzania wote kwa ujumla tunapaswa kujiuliza swali hili, ni Tanzania ipi tunayoitamani? Jibu sahihi ni Tanzania yenye nguvu ya kiuchumi. Ili Tanzania ifikie kuwa Taifa la uchumi wa kati na Tanzania ya viwanda ni lazima na muhimu kupanua wigo katika sekta ya kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hotuba yangu ya leo ya Wizara ya Kilimo, nitaongelea suala moja tu nalo ni zao la tangawizi. Nianze kwa kuuliza swali ambalo nitalijibu sawia. Tangawizi ni zao gani? Ni zao ambalo ni jamii ya viungo (spices). Pili, tangawizi ni malighafi ya kutengeneza madawa ya binadamu, vipodozi, vinywaji na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitaongelea tangawizi kiulimwengu, Afrika na Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kiulimwengu; ukisoma vitabu vya zao la tangawizi ulimwenguni utaona kwamba mataifa tano bora yanayoongoza ulimwenguni kwa kulima zao la tangawizi ni India, China, Nepal, Nigeria, Thailand. Nchi hizi tano bora kwa kilimo cha tangawizi zimeweza kujiboresha kiuchumi kupitia zao hili la kilimo. India inalima asilimia 34.6 ya tangawizi yote inayolimwa duniani, inaongoza kwa kulima tangawizi na pia inaongoza kwa kuitumia. China inalima asilimia 19.1, Nepal inalima asilimia 10.1, Nigeria inalima asilimia 7.8, Thailand inalima asilimia 7.8. Nchi nyingine zinazojitahidi ni Indonesia, Bangladesh, Japan, Cameroon na Taiwan hizi zinaingia kwenye kumi bora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nisiishie hapo nchi tano ulimwenguni zinazoongoza kwa ku-export tangawizi aidha ikiwa mbichi (raw ginger) au ikiwa imesindikwa, kwa takwimu hizi za mwaka 2015 China inaongoza kwa ku-export asilimia
39.9 ya tangawizi yote iliyouzwa duniani, India inashika nafasi ya pili kwa ku-export asilimia 14.5 japo inaongoza kwa kulima tangawizi duniani lakini inaongoza kwa kutumia tangawizi pia. Nigeria inashika nafasi ya tatu kwa ku-export tangawizi duniani na ina-export asilimia tisa ya tangawizi inayofika kwenye soko la duniani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa moyo wa unyenyekevu mkubwa, kwa moyo uliopondeka nitoe shukrani zangu za dhati kwa wafuatao:-

Bodi ya Wadhamini wa LAPF na Mkurugenzi wa LAPF kwa kumuunga mkono Mheshimiwa Rais wetu mpendwa Dkt. John Pombe Magufuli katika jitihada zake za kuijenga Tanzania mpya ya viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, LAPF wameingia ubia na kiwanda cha kusindika tangawizi cha Miamba Same Mashariki kupitia kampuni yake ya Mamba Ginger Company Limited. LAPF kuingia ubia na kiwanda cha kusindika tangawizi kuna yatokanayo yafuatayo:-

(i) Walima tangawizi wa Wilaya ya Same na Tanzania nzima watapata soko la uhakika la kuuza tangawizi yao.

(ii) Ni dhahiri kwamba kilimo cha tangawizi Tanzania kitapanuka na haswa kama Serikali itajali kujenga miundombinu endelevu kwa wakulima tangawizi.

(iii) Ni dhahiri kwamba tangawizi sasa tutaingia kwenye biashara ya uhakika ya kuuza tangawizi nje ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina uhakika na haya ninayoyasema kwamba walima tangawizi wa Tanzania wanapata taabu sana inapofikia kwenye kupata soko la zao kwa walanguzi ambao wanawapangia bei.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tangawizi inastawi sana Same Mashariki na mpaka sasa hivi ninapoandika hotuba hii ardhi ya Same Mashariki ililimika tangawizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania tunayo mikoa yenye ardhi nzuri sana yenye rutuba kama ile ya Nigeria. Mvua ya kutosha, climate condition nzuri; mito isiyokauka. Mikoa hiyo kwa uchache wake niitaje ni pamoja na Ruvuma, Mbeya, Iringa, Rukwa, Kigoma, Arusha na Kilimanjaro.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tangawizi sasa hivi imeonesha mwamko wa Watanzania kuanza kulima zao la tangawizi. Napata simu nyingi sana kutoka Kigoma wananchi wakinipa simu kuhusu wapi wanauza zao lao la tangawizi. Songea vijijini Jimbo la Madaba wananchi wameanza kilimo cha tangawizi tangu mwaka 2012. Mimi nahamasisha sana kilimo cha tangawizi nami nikiri kwamba nimewekeza katika kilimo cha tangawizi na nimeanza na ekari 20 nalima tangawizi Madaba, Songea Vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naisihi sana Serikali ifanye kila jitihada kuliangalia zao hili la tangawizi kwani iwapo Serikali itajihusisha kikamilifu tutakuwa tunatengeneza zao litakaloweza kutuingizia fedha za kigeni. Leo hii nchi ya Nigeria inachangia asilimia tisa ya tangawizi yote inayouzwa kwenye soko la dunia na matumizi ya tangawizi kiulimwengu yamepanda kwa asilimia takriban asilimia 7.5