Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo ni uti wa mgongo, pia Tanzania tunategemea sana kilimo katika maisha ya kila siku. Naomba Serikali iwezeshe tuwe na viwanda vya kusindika vyakula, viwanda vya nyama, viwanda vya samaki, matunda, juisi na viwanda vya maziwa ya ng’ombe. Tukiwa na viwanda, vijana wetu watapata ajira katika viwanda hivyo. Kwa hiyo, kuwa na viwanda vinavyotumia nafaka ya kilimo tunaweza kuendelea na kukuza uchumi kwa wananchi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri kwamba Serikali ipeleke mbolea kwa wakulima kwa muda unaotakiwa. Jimbo la Mufindi wakulima wanaanza kulima kuanzia mwezi wa Tisa hadi mwezi wa 11. Muda huo ndiyo mbolea inatakiwa kwa wakulima wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali kupanga bei ya mbolea ambayo mkulima mdogo anaweza kumudu kununua kwa bei ya chini. Pia naomba Serikali ilipe madeni ya Wakala wa Mbolea. Wapo watu ambao wanaidai Serikali kwa sababu walikopa kwenye mabenki ili kuongeza mitaji yao, basi naomba Serikali iwalipe hao mawakala wa mbolea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile naomba Serikali ipeleke matrekta ili kulima kilimo cha kisasa. Matrekta yatasaidia sana kukuza kilimo katika nchi yetu. Pia iwepo mikopo ya pembejeo kwa wakulima wadogo wadogo. Kuwepo na vikundi vinavyojihusisha na kilimo, uvuvi na ufugaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na naunga mkono hoja.