Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Kigoma Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. KABWE Z. R. ZITTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Ibara 106 katika ukurasa wa 68 wa hotuba inayozungumzia mazao yanayozalisha mafuta ya kula, Mkoa wa Kigoma ni mzalishaji mkubwa wa mawese na uzalishaji wake unaweza kusaidia nchi kupunguza uagizaji kutoka nje. Mkoa wa Kigoma umeandaa mkakati wa kuendeleza zao la michikichi na kupitishwa na RCC ya Mkoa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali Kuu ishirikiane na Halmashauri za Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma ili kuwezesha utekelezaji wa mkakati huu. Tunategemea kuwa wakulima wadogo 100,000 wenye hekta moja kila mmoja watahusika na uzalishaji wa mawese na hivyo kukuza viwanda mkoani Kigoma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba zao la mawese lisisahaulike, ni ukombozi kwa Mkoa wa Kigoma. Kuna fedha kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika kwa ajili ya mazao ya mafuta ya kule. Wizara ishirikiane na Sekretarieti ya Mkoa wa Kigoma kufanikisha hili. Manispaa ya Kigoma Ujiji inaomba msaada wa kununua miche milioni moja ili kuweza kupanda kwenye msimu huu wa kilimo kuanzia Novemba. Tunaomba Wizara ishirikiane na sisi kufanikisha mradi huu wenye ukombozi mkubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu hifadhi ya jamii kwa wakulima, naishauri Serikali kupanga sera na baadaye sheria itakayowezesha wakulima kuwa na hifadhi ya jamii. Nimeona mafanikio ya wakulima scheme ya NSSF. Hata hivyo, tunaweza kuwa na wakulima wengi zaidi kwenye hifadhi ya jamii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tutungie sheria suala hili ili mafao kwa wakulima yawe ya kisheria. Fao la bei itakuwa ni ukombozi mkubwa sana kwa mkulima. Hifadhi ya jamii inaendelea na kuwepo kwa fao la bei.