Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Mussa Bakari Mbarouk

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Tanga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Mwenyekiti, naanza kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijaalia afya njema na kuniwezesha kuchangia. Naunga mkono hoja ya hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani katika kuchangia bajeti ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kupitia Waziri Kivuli, Mheshimiwa Cecilia Paresso.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naungana na Kamati ya Kilimo katika maoni na ushauri ilioutoa katika kitabu chake ukurasa wa tatu. Inashangaza kuona wafadhili wanatoa fedha nyingi kufadhili kilimo kuliko Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ili tuendelee tunahitaji mambo manne; moja, ardhi – kilimo, ujenzi, ufugaji, viwanda, barabara na kadhalika; pili, watu – wakulima, wafanyakazi na wafanyabiashara; tatu, siasa safi - kwa kuwa haipo; nne, uongozi bora – hakuna sababu. Uongo na mipango isiyotekelezeka. If you fail to plan, you plan to fail.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania tupo hapa kwa kuwa plans zetu zote tume-fail na tunapeleka mambo kisiasa ili kuvutia wapiga kura. Asilimia 75 ya Watanzania ni wakulima. Wizara hii ni nyeti na ni uti wa mgongo wa Taifa letu, inachangia 29% ya pato la Taifa letu na inatoa ajira 75% ya watu wetu. Kwa masikitiko makubwa, bajeti iliyotengwa ni 3.0%. It is the shame, hapa Serikali inafanya utani na kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha zilizotengwa katika bajeti; wafadhili 78%, fedha zetu 21%. Fedha zilizotengwa katika bajeti, shilingi bilioni nne mifugo, shilingi bilioni mbili uvuvi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mkanganyiko/ ugumu katika taasisi za fedha; wakulima ni wachangiaji na wazalishaji wakubwa katika uchumi wa Taifa letu, lakini ndio wanadharauliwa mno na Serikali haina mission wala vision. Wakulima katika benki wamewekewa masharti magumu, pamoja na kuwa na hatimiliki za ardhi, nyumba na vyombo vya moto. CRDB (Co-operative and Rural Development Bank) enzi za Mwalimu (by definition) ilikuwa ndiyo benki yao wakulima. Je, leo CRDB ni ya wakulima? Ni ya wafanyabiashara na wawekezaji. Yamewekwa mazingira na dhana kuwa wakulima hawakopesheki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo ni kizungumkuti, Tanzania haijaamua kutoa kipaumbele katika kilimo (first priority) kwa kuwa kilimo kinaendeshwa kisanii kwa matambo na misamiati mingi na siasa kibao:-

(i) kilimo cha kufa na kupona;

(ii) kilimo cha ujamaa na kujitegemea;

(iii) kilimo ndio uti wa mgongo wa uchumi wa Taifa letu,

(iv) kilimo cha bega kwa bega; na

(v) kilimo kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, kwa misamiati hii ndiyo tutavuna mahindi, mpunga, viazi, mtama, ngano, alizeti, pamba na karafuu? Serikali ijipange na tusiwe wababaishaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu tumbaku na soko la nje, kilogramu 32,000 ni sawa na 3.2 tonnes iliyouzwa Uturuki kutoka Tanzania. Nchi nyingine wanaolima tumbaku wameuza tumbaku kilogramu 939,000,000, Uturuki (Europe). Hii inadhihirisha namna gani Serikali haiko serious katika mambo ya kiuchumi tofauti na nchi za jirani, Mozambique, Rwanda, Kenya, Uganda, na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanga na zao la mihogo na matunda. Tanga ni wazalishaji wakubwa wa mihogo hususan katika maeneo ya vijijini. Mfano, maeneo ya Kirare, Mapojoni, Pongwe, Kisimatui, Marungu, Mkembe, Mpirani, Mabokweni, Putini, Bwagamoyo na kadhalika. Mihogo ya Tanga ni mihogo bora, mitamu na haina sumu ukilinganisha na mihogo ya maeneo mengi katika Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mihogo ya Tanga haina soko la uhakika ndani na nje ya Tanzania. Siku za karibuni China walitoa tangazo (tender) kwa kutaka zao la muhogo katika mitandao/media. Je, Serikali ya Tanzania, Mheshimiwa Waziri anatuambie? Wamelifuatilia soko hilo vipi? Wamefikia hatua gani ya majadiliano?

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee kuhusu uvuvi na siasa za Tanzania. Norway ni nchi tajiri na mfadhili mkubwa katika miradi mingi ya kimaendeleo Tanzania na Afrika nzima. Utajiri wao unatokana na uvuvi ambao wameamua kuwekeza, kutafiti na kushughulika kikamilifu. Tanzania tunazo 1,400 cubic kilometres (Indian Ocean) kutoka Jasini – Mkinga – Tanga hadi Msimbati – Mtwara; ni bahari tupu na kuna samaki wa kila aina. Humo Indian Ocean kuna gesi pia, lakini Watanzania (Coastal zone are very poor people), ndio maskini wa kutupwa. Badala ya Serikali kuwasaidia, vyombo na nyavu zao zinachomwa moto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu kwa Serikali ni kwamba Serikali ithamini watu wa Ukanda wa Pwani katika Mikoa ya Pwani, Tanga, Dar es Salaam, Lindi, Mtwara, Unguja, Pemba na Mafia kwa kutafuta wawekezaji (investors) wa viwanda vya kusindika samaki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vijengwe vyuo vya uvuvi kwa ajili ya elimu ya uvuvi wa kisasa. If you fail to plan, you plan to fail. Jambo lolote likifanywa kitaalam (kielimu) linakuwa na manufaa makubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uvuvi (registration fees 20,000 under 20mt boat); Serikali iondoe tozo/kodi ambazo ni kero kwa wavuvi. Tukiachilia mbali kodi iliyoondolewa kwa vyombo vyenye urefu chini ya mita 20, lakini bado Halmashauri inatoza tozo na Serikali Kuu inatoza tozo ya leseni kwa kila baharia. Leseni alipe nahodha tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, katika vyombo vingine kama bus, anaulizwa leseni dereva na siyo conductor wala turn boy? Kwani wavuvi ni wote?

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika meli meli/ferry boat anahojiwa captain tu. Kwa nini wavuvi wanatozwa leseni? Samaki wao wanatozwa ushuru na vyombo vyao registration fees na kodi ya mapato (revenue). Matrekta hayana kodi, lakini mashua zina kodi kubwa. Badala ya kukamata vyombo na nyavu za wavuvi wadogo na kuzichoma (hasara), wazuie utengenezaji wa nyavu ndogo katika viwanda vyetu na iache kuchukua kodi na itoe vipimo vya nyavu (size) zinazohitajika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri kwamba kwa kuwa mara kwa mara wakati wa kaskazi ajali nyingi hutokea, hivyo Serikali iwe na Rescue Team Department isaidie kuokoa ajali zinapotokea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa mifugo, kuna usafirishaji katili, wanyama wengi wanateswa/kufa katika usafirishaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna gharama kubwa za dawa kwa ajili ya kilimo na mifugo. Wanyama hawatendewi haki Tanzania kwa sababu hakuna chama cha kutetea haki zao. Wanyama kama ng’ombe, mbuzi, kondoo na kuku wanasafirishwa katika vyombo vidogo na wanabanana na kuumia hadi kufa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri kwamba Wizara iliangalie suala hili kwa umakini kwa kuwa hata wanyama wetu wanakosa soko bora kwa kuwa nyama yao huwa na dosari.