Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi


MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumpongeza Mheshimiwa Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Mheshimiwa Charles Tizeba pamoja na Naibu wake Mheshimiwa William Tate Olenasha kwa kazi nzuri katika Wizara hii. Naomba pia nimpongeze Katibu Mkuu wa Wizara Eng. Mathew Mtigumwe pamoja na timu ya watendaji wa Wizara hii kwa jitihada zao. Hata hivyo ninayo machache:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru Katibu Mkuu kwa hatua alizochukua za kuhakikisha kuwa wakulima wangu wa kahawa wanalipwa. Pili, tunapongeza Wizara kwa kuweka kipaumbee katika zao la korosho na hivyo kutoa ruzuku katika pembejeo za madawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Nyasa ni wakulima wa kahawa na uvuvi. Kwa upande wa wakulima Serikali imekuwa ikiwapa support ya kuwajengea maghala na pembejeo za mbolea (ruzuku).

Mheshimiwa Mwenyekiti, upande wa wavuvi mazingira yao ya uvuvi ni duni sana. Mialo imekuwa na vibanda duni na hata mitumbwi yao ni duni. Wavuvi hulazimika kumwaga dagaa ziwani wakati wa mvua kwani hawana drying shed. Serikali ina mpango gani wa kuwainua kundi hilo kwa kurekebisha mazingira yao ya biashara?

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la samaki wanaoitwa vituwi, wavuvi wa nyasa wanasikitika kuwazuia kuvua samaki hao kwa kutumia nyavu za saizi ndogo, wao wanadai kuwa samaki hao hawakui. Naomba ufanyike utafiti juu ya suala hilo. Nitanyimwa Ubunge kwa ajili ya vituwi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Zao la mihogo; Wilaya ya Nyasa Kata ya Kihagare bado ina mihogo ya asili (Gomela) ambayo ina ladha nzuri sana. Baada ya kuleta mbegu za kisasa wakulima wengi walihamasika kwa mbegu mpya, lakini katika kuchemsha ladha ya mbegu mpya haina uzuri kama gomela. Matokeo yake Gomela imesababisha utamaduni wa wizi. Ukipanda Gomela iwe katikati, pembeni, vyovyote vile ikikua lazima iibiwe. Mimi pia niliibiwa. Naomba Wizara ifuatilie mbegu hiyo ili isipotee, ni mbegu nzuri sana na inaweza kufaa zaidi hasa kwa kitafunwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ruzuku za injini za boti, utaratibu ukoje? Kwa nini zisitengwe fedha za kuleta maboti ya mbegu ili kuwasaidia wavuvi kununua yakiwa jirani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nazidi kuwaomba kutembelea Jimbo langu la Nyasa. Nawatakia kazi njema.