Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Daniel Edward Mtuka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. DANIEL E. MTUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, TAKUKURU ni chombo ama Taasisi simamizi ambayo ikijengwa vizuri itasaidia sana kudhibiti rushwa, wizi, ubadhirifu na hivyo kupandisha GDP. OC haihusu mishahara bali ni kugharamia mafuta ya magari kuwapeleka Maafisa wa PCCB kufuatilia wahalifu, kutembelea miradi ambayo ipo chini ya viwango, rushwa katika idara mbalimbali, kutoa elimu ya mapambano dhidi ya rushwa na kuendesha kesi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nchi tumekubali kuwa rushwa ni adui namba moja Tanzania na hatuwezi kuistahimili (zero tolerance) ni lazima tupambane nayo. Hatukatai kwa Serikali kubana matumizi na kuzipeleka kwenye miradi ya maendeleo lakini hatuwezi kukwepa kuitengea fedha ya operesheni.
Mheshimiwa Naibu Spika, udhibiti wa rushwa ni vita kubwa, tunahitaji kuwaweka na kuwapa kila aina ya support TAKUKURU ili wafanye kazi inavyotakiwa. Bajeti ya mwaka huu waliyotengewa kwa maana ya OC inanivunja moyo kwamba mapambano dhidi ya rushwa hayatakuwa precise.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano, bajeti ya OC ya TAKUKURU kwa miaka mitano ni kama ifuatavyo:-
Mwaka 2012/2013 shilingi bilioni 15.5; mwaka 2013/2014 shilingi bilioni 15.5; mwaka 2014/2015 shilingi bilioni 16.5; mwaka 2015/2016 shilingi bilioni 14.2; na mwaka 2016/2017 shilingi bilioni 12.06.
Mheshimiwa Naibu Spika, naishauri Serikali yangu iongeze OC kwa TAKUKURU ili ifanye kazi ya udhibiti. Sasa hivi mbinu za wala rushwa zimebadilika, idadi ya wahalifu imeongezeka kutokana na hali ya maendeleo ya nchi, watumishi wa TAKUKURU pia wameongezeka na thamani ya fedha imeshuka, hivyo kitendo cha mwaka 2012/2013, OC kupata fedha nyingi kuliko bajeti ya mwaka huu imeniogopesha sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha na naunga mkono hoja.