Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia kwanza kuhusu wakulima wa chai Rungwe. Kumekuwa na migogoro mingi sana kati ya wakulima wa chai Mkoa wa Mbeya, Wilaya ya Rungwe na wadau wa chai akiwemo Mohamed Enterprises na WATCO kwani bei ya chai ni ndogo sana na baadhi ya wakulima kujiondoa katika uuzaji wa chai katika viwanda vya Katumba na Busokelo kwa madai ya maslahi madogo na wakati huo huo Bodi kuzuia kuuza kwa chai na kampuni ya Mohamed Enterprises na kuzuia uhuru wa kibiashara ambapo mwisho wa siku mkulima ndiyo hunufaika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili mazao kuuzwa kwa ujazo wa lumbesa. Naomba Wizara iweke mkazo na msisitizo wa kusaidia wakulima wanapouza mazao kulazimishwa kujaza mazao katika mfumo wa lumbesa kwani wakulima hupata hasara kubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, naomba niongelee kuhusu pembejeo zisizo bora. Kumekuwa na malalamiko ya pembejeo zisizo na kiwango na kupelekea makusanyo duni na kuwapa hasara wakulima wetu hasa wa Mkoa wa Mbeya. Serikali ina mkakati gani wa kusaidia wakulima hawa na pia kuchukua hatua kwa wahalifu wote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nne, niongelee kuhusu bei ndogo za mazao. Wizara inasaidiaje wakulima wauze mazao yao kwa bei ya faida ambayo itasaidia kulipa gharama za kilimo walichowekeza na kudhibiti madalali wanaopata pesa nyingi kuliko wakulima wenyewe?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tano, Kituo cha Kilimo Uyole. Kituo hiki ni muhimu sana kwa wakulima wa Nyanda za Juu Kusini kwani utaalam wao unahitajika lakini cha kushangaza pesa inayotengwa kwa shughuli za maendeleo haziwafikii kwa wakati na hata wakati mwingine kutofika kabisa na kukwamisha shughuli za kitafiti na kiutendaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sita ni kuhusu wakulima na wafugaji. Tunaomba ufumbuzi wa kudumu juu ya wakulima na wafugaji utafutwe ili kupunguza/kuondoa ugomvi kati ya jamii hizi.