Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. ANGELINE S. L. MABULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuunga mkono hoja na niwapongeze kwa kazi nzuri pamoja na changamoto zote wanazokumbana nazo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, nishauri tu katika kuboresha sekta ya uvuvi ni vyema season fishing ikapewa kipaumbele, italeta tija sana katika sekta hii. Tuyatambue mazalia ya samaki na kisha tuweke programu maalum ya kutekeleza season fishing.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, tutoe kipaumbele katika cage fishing. Tuwekeze kwa vijana ili ufugaji wa samaki ufanyike katika mfumo wa kuwa na plot ndani ya ziwa ama bahari kwa kuweka wigo katika maeneo yatakayowekezwa katika uvuvi kwa njia ya uvuvi wa wigo ziwani ama baharini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, kuhusu ufugaji wa ng’ombe ni vyema wafugaji/wachungaji wakashauriwa kufuga ufugaji wa kitaalam na kuwaelekeza wafugaji wetu kufuga kitaalam ili wawe na tija katika ufugaji wao badala ya kuwa na ufugaji wa kuhamahama kitendo ambacho kinachangia sana katika kuleta migogoro ya wakulima na wafugaji.