Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nishukuru sana kunipa nafasi ya kuchangia. Awali ya yote, niipongeze sana Serikali kwa kuja na mfumo mpya wa uagizaji mbolea. Eneo hili nawapongeza sana kwa sababu ndiyo eneo ambalo litawasaidia sana wakulima wa nchi hii ili kuepukana na mfumo uliokuwepo zamani uliokuwa unawanufaisha wachache. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda niiombe Serikali isirudi nyuma na nimwombe Waziri, najua anafanya kazi ambayo itakuwa ngumu sana, wapo watu ambao walikuwa wananufaika na biashara hii kwa hiyo ni vizuri wakajipanga wasirudi nyuma. Naamini kuleta mbolea kwa pamoja litapunguza gharama kubwa sana ya bei ya pembejeo na pale ambapo atakuwa amekwama zaidi tutahitaji sana kumsaidia ili tuweze kusonga mbele na kuwasaidia Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye eneo hili nashauri, hata zile mbolea za NPK, KANI na SA zina uwezekano kabisa wa kuweza kuisimamia Serikali ikaweza kuagiza mbolea hizi, upo uwezekano. Naamini tu tukifanya jitihada za pamoja wakishirikisha na wadau wataweza kusaidia zoezi hili likakamilika na likawasaidia wananchi wote kwa ujumla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ambalo napenda kuchangia ni suala la tozo ambalo limeletwa na Serikali. Tunaipongeza sana Serikali imetengeneza mazingira mazuri ya kuboresha mazao karibu yote kwa kupunguza zile tozo ambazo zilikuwa ni kero kwa wakulima wetu. Kuna maeneo ambayo zipo tozo zimeelekezwa hasa kwenye vyama vya ushirika, ni vyema wakaziangalia kwa undani zaidi tozo hizo kwani kuna baadhi ya maeneo wanaweza wakaviua vyama vya ushirika, vyama vya ushirika vinategemea sana tozo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naamini kwa umahiri alionao Waziri atawashirikisha wadau kabla ya utekelezaji ili waangalie vile vyama visije vikafa kwa sababu ukiua vyama vya ushirika havina nafasi ya kuweza kushindana na makampuni. Vyama vya ushirika pekee ndivyo ambavyo vikiungana vina nafasi ya kuweza kutoa ushindani kwa haya makampuni ambayo yananufaika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini zipo tozo ambazo zimeonesha wazi kwamba zinayasaidia makampuni ili yapunguze gharama sasa naomba Waziri aangalie tozo zile. Tunaweza tukatoa hizi tozo zikawasaidia makampuni moja kwa moja bila kwenda kwa mkulima. Ni vyema wakaangalia na wakachambua zile tozo mbalimbali ili zingine ziwarudie wananchi na kufanya zao liweze kuwa na bei nzuri kuliko tukitoa tu nafuu ni ya kuyabeba sana makampuni. Niombe sana hili waliangalie na naamini wataalam waliopo watasaidia kuchambua zile tozo ili ziweze kusaidia wananchi kama Serikali ilivyokusudia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ni kwenye sekta ya uvuvi, kwangu kuna Ziwa Tanganyika ambalo kimsingi bado sekta hii haijafanya kazi vizuri sana. Tunaiomba Serikali iwasaidie wale wavuvi wa wadogo wadogo iwape mazingira ambayo yatawawezesha kufanya shughuli zao za uvuvi bila kupata shida. Ni vizuri tukaangalia vile vikundi vya wavuvi vikasaidiwa na Serikali ili viweze kutengeneza tija.
yangu ya Tanganyika tulileta maombi maalum ya kulima zao la pamba. Tayari wakulima walishafanya jitihada zao, wameonesha nia njema na nimshukuru alinipa ushirikiano na kuagiza wataalam wakaenda kuangalia jitihada ambazo zimefanywa kule. Kwa hiyo, nina imani eneo hilo tunahitaji kibali tu kwa msimu ujao ili wakulima wale waliojipanga waweze kulima lile zao liwasaidie na kuongeza kipato kwani watakaponufaika kwenye eneo hili litawasaidia sana kwa Serikali na wananchi kuongeza kipato.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa bado kuna dakika moja, naomba niongelee sana miradi ya uwamgiliaji.
Nchi yetu ili iweze kwenda inahitaji sana…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)