Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

Hon. Sixtus Raphael Mapunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi name nichangie kwenye uti wa mgongo wa Taifa letu la Tanzania. (Makofi)

Awali ya yote nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri, muda wote nilipokuwa nauliza maswali ya msingi na ya nyongeza kuhusu kero zinazowakabili wakulima wa kahawa kwenye tozo nyingi zisizoeleweka, leo wamelijibu hili kwa kuondoa tozo 17. Tulipokuwa tunapigania zile tozo zitoke kwenye 26 na 27, tulitambua kwamba kati ya vitu vinavyomkwaza mkulima wa kahawa kule chini, ni bei ndogo iliyosababishwa na tozo nyingi zilizokuwa katikati ya mchakato, yaani kutoka kwa mkulima mpaka unafika juu kwa mnunuzi mnadani na nje ya mnada. Sasa mmelifanya hili jambo kubwa sana na kuna wachache watabeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawaomba kwenye hili Serikali mmefanya jambo zuri na ongezeni moja lingine. Kwa sababu mmeziondoa zile 17, msiache hewani, wekeni na bei ya kiwango cha chini cha ununuzi wa kahawa. Kwa sababu



kwenye tafiti zetu tunajua, hizo dola zote zilizopungua zimeondoa gharama za uendeshaji, uzalishaji na gharama za usafiri na kitu kingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ili tumsaidie mkulima kule chini tufanye kama tulivyofanya kwa mahindi mwaka 2016, tukasema mtu asinunue mahindi ya mkulima mpaka awe na shilingi 500 kwa kilo ndiyo yanunuliwe. Kwenye kahawa, korosho, tumbaku na kwenye pamba tunaweza tukafanya hivyo hivyo. Tukifanya haya ninayoyasema, ule wasiwasi aliokuwa nao ndugu yangu Mheshimiwa Silinde utakuwa umeondoka. Kwa kweli tutakuwa tumemsaidia mkulima, ila tunafahamu gharama zilizokuwa katikati ya mchakato zilikuwa zina-trickle down zinafika zinamsumbua mkulima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee suala lingine kuhusu ukuaji wa kilimo na Tanzania ya viwanda. Tutaongea hapa siku zote kuanzia asubuhi mpaka jioni, tusipo-link hizi sekta mbili; sekta ya kilimo na sekta ya viwanda, mambo yote mawili hayataweza kwenda. Kwa nini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunasema tunataka tumsaidie mkulima aliyelima nyanya zake zikaoza pale Dumila kabla hajafika kwenye soko, anahitaji katikati kitu kinaitwa processed Industry ili kwanza kuongeza value ya zile nyanya zake, lakini kuzitunza ili zisiweze kuharibika. Pale anahitaji awe na kiwanda. Utaongelea korosho, the same, utakwenda kwenye mahindi, tutazalisha mahindi ya kutosha, lakini tusipoyaongezea ubora wa kutosha tutapata tatizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hakuna maendeleo ya viwanda kwenye Taifa la Tanzania bila kuwa na maendeleo ya kilimo, vyote vinakwenda pamoja. Utakwenda kuongelea habari za ufugaji, utaongelea masuala ya ngozi hapa, mimi mpaka nashangaa. Hivi kweli tunashindwa ku-intervene tukapata kiwanda kimoja hata kwa mkopo kwa ajili ya ku-process bidhaa zinazotokana na ngozi, halafu wafugaji wetu wakawa na ahueni kwenye maisha yao? Kweli hili linashindikana.

T A A R I F A . . .

MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana Mheshimiwa Kanyasu. Kimsingi hiyo taarifa ana- compliment kwa ninachokiongea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunachohitaji, we need a serious government intervetion kwenye vitu kama hivi. Kama kiwanda kilikuwepo, vilikuwepo vingi, sitaki kurudi nyuma. Nilichotaka nikiseme hapa kwa nia njema, tukitaka tutoke tuisaidie Sekta ya Kilimo, tunahitaji a serious intervetion kwenye kuwekeza kwenye kilimo. Kwenye mambo yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza, lazima tuichore tena ramani ya kilimo ya nchi yetu including watalaam wa research, wafanye tafiti. Ukiangalia Morogoro, ina sifa kubwa ya alluvial soil. Alluvial soil ni udongo wenye rutuba na Mkoa wa Morogoro tukiungalia unapata mvua bila matatizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiondoa mvua, bado una mito mikubwa inayoweza kufanya Morogoro peke yake ikafanya Tanzania isife njaa. Kwa nini nasema hivyo? Kwa sababu Serikali hapa haija-invest kwa huyu mkulima, inadhani mkulima anajua. Mkulima hajui. Hapa lazima tumwambie mkulima cha kufanya, namna ya kufanya na namna gani tutatoka hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mvua zilizopita zimetuletea mafuriko lakini mafuriko yale kwa wenzetu ni neema. Hebu tujiulize tungeweka mabwawa ya kuyaelekeza yale maji ya mafuriko kipindi hiki ambacho wakulima hawawezi kulima na wakilima mvua zinazidi mazao yanaharibika, tungeyateka yale maji tungeweka katika maeneo ya mabwawa, kipindi cha mwezi wa Sita, wa Saba ambapo mvua hakuna, maji yale yale ambayo yalitukwaza sasa yatumike kwenye kilimo. Vitu kama hivi vinahitaji tu kuelekezwa, Serikali elekezeni tu kila kitu kitafanyika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine mnaongea irrigation, irrigation, irrigation, kuna njia rahisi sana za kuifanya Tanzania iwe ya umwagiliaji. Tuna utaratibu tumeuweka hakuna shule ya sekondari, shule ya msingi itakayojengwa bila choo, tunashusha tu circular, hakuna shule yoyote ya msingi na sekondari itakayojengwa bila kuwa na miundombinu ya kuvuna maji ya mvua. Ukivuna maji ya mvua from day one mtoto akiwa shule ya msingi anajifunza umwagiliaji kutokana na maji ya mvua. Sasa sijui tumelogwa, hata sijui tufanyeje lakini ninachoweza kusema hapa kwa kweli Serikali inahitaji serious intervention kwenye hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sehemu nyingine huwezi ukakuza sekta ya kilimo bila kuwa na uhakika wa matumizi bora ya ardhi. Douglass Jerrold katika andiko lake la “A land of Plenty” alitumia methali moja ya kilatini, alisema “Cujus est solum, ejus est usque ad coelum” akimaanisha “He who owns the soil or land owns up to the sky” kwamba matumizi bora ya ardhi ni utajiri mkubwa kuliko kitu kingine chochote. Nchi yetu tumebarikiwa kuwa na ardhi bora, kinachotusumbua sisi kila siku tunadhani tunaanza upya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimuulize swali moja Mheshimiwa Waziri anaikumbuka Kapunga Rice Project? Project ambayo ilikuwa kuwa ya irrigation scheme, iliandaliwa kwa ajili ya kuwasaidia watu, ukifika pale kwa sababu maji yapo, mkulima ana uhakika wa kuvuna. Nenda pale Morogoro kuna ile Dakawa Rice Project nayo ni irrigation system nzuri, kama Serikali ilishawekeza watu wananufaika pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuichore ramani ya Tanzania kwa maeneo sita au saba ya kuanzia kama tulivyofanya Dakawa, tufanye vilevile Kilombero, tufanye hivyo kwa Mheshimiwa Mwamoto kwenye lile Bonde la Mto Ruaha wanalima vitunguu vizuri sana kule, wawekewe utaratibu uleule wa irrigation haya mambo yote yatakwisha tutakuwa hatuna matatizo na twende maeneo ya Rungwe kule kuna mifumo mizuri ya kilimo kuanzia Januari mpaka Disemba. Tusipofanya a serious intervention kwenye kilimo hatutatoka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo ambalo naweza nikashauri ili twende vizuri, tunataka tuwasaidie wakulima, wakulima tukiwaacha na hekari moja moja hatutafanikiwa. Jambo la kufanya, wale wote ambao wanalima kwenye eneo linaloelekeana tufanye mechanization of agriculture. Kama mtu ana hekari mbili kijiji kizima mna jumla ya hekari 10,000, hizi hekari 10,000 zote zinakuwa communal tuna-inject pale trekta na taaluma, kwa hiyo, kila mwenye hekari yake moja ana-offer labour kwenye ardhi yake ili tupate tija kwa sababu hatuna uwezo wa kila mmoja kuwa na trekta.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi ndivyo kilimo kilivyokuwa duniani kote, hatuwezi tukaendelea na hii asilimia 65 hapa tunajidanganya. Asilimia 65 ya hekari moja moja tunalima nini? Mimi hapa nimepata magunia mawili, mwingine matatu halafu tunajiita wakulima, we are not…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante.