Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. JOHN C. KANYASU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Naomba niseme kwa kifupi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, naomba niwaombe wahusika Mfuko wa Jimbo bado unakwenda Halmashauri ya Wilaya hauji Halmashauri ya Mji walishughulikie.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini suala la TASAF, tatizo lililosemwa na Wabunge wengine liko kwangu pia, naomba litazamwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye Kamati yangu ya UKIMWI tulikutana na Group of Donors, wanasema ufadhili unaendelea kupungua na wanaitaka Serikali kuongeza uwezo wake kwenye mfuko wa AIDS Trust Fund. Kwa sababu kadri wanavyoonesha inaonekana mwaka huu itapungua zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, tuliambiwa hapa kwamba jukumu la Ofisi za Wabunge liko chini ya TAMISEMI kwa maana ya Ofisi ya Waziri Mkuu. Tunaomba watoe maelekezo tunapotoka hapa tupate ofisi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme lingine, katika Hospitali yangu ya Wilaya ya Geita kuna madeni ya watumishi ya tangu mwaka 2007. Madeni hayo yamefanyiwa uhakiki zaidi ya mara tatu lakini fedha hizo haziendi na hawalipwi. Nilitaka kufahamu kwenye bajeti hii kama fedha hizo zimetengwa na wataanza kulipwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia katika Hospitali yangu ya Wilaya ya Geita yalifanyika mazungumzo ya Serikali ya Mkoa pamoja na mfadhili COTECNA, ambaye walikubaliana kujenga diagnostic centre. Baada ya mabadiliko haya ya Mkuu wa Mkoa yule mfadhili amekwishaandaa fedha anakwenda pale anasema waliopo wote hawatoi ushirikiano. Naomba sana apewe ushirikiano. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lipo tatizo la ukusanyaji wa service levy. GGM wanatoa orodha ya kampuni 1,000 wanazofanya nazo kazi lakini 90% ya hizo kampuni ziko nje ya nchi. Nilitaka kupata mwongozo hizo kampuni zilizoko nje ya nchi ambazo GGM hawataki ku-disclose kwamba zinatoaje service levy, tunazipataje hizo fedha Halmashauri ya Mji wa Geita? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Kamati yangu tulitembelea Buhangija, tukaenda kwenye kituo cha watoto albino. Tulipofika pale tulikuta kuna taarifa kwamba wake wa viongozi walifanya harambee kuchangia kituo kile miaka miwili iliyopita lakini fedha hizo hazijawahi kufika na tulikuwa na Naibu Waziri, Mheshimiwa Dkt. Possi. Tunaomba kujua waliofanya harambee hizo fedha zilikwenda wapi? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba pia kuchangia kwenye suala la ujenzi wa ofisi. Nchi hii kila Halmashauri ina ramani yake, nataka kushauri pawe na common ramani ya Halmashauri zote. Halmashauri yangu ina fedha za kujenga ofisi miaka minne sasa fedha ziko ndani, ofisi haijengwi na kwa taarifa zilizopo wamepunguza karibu shilingi milioni 300 kuchoresha ramani mpya. Mkuu wa Mkoa aliyekuwepo alikuwa amewaletea ramani ambayo tayari imechorwa na imejengwa sehemu zingine. Naomba Mheshimiwa Waziri afuatilie ili Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya iweze kujengwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, kwa sababu ya muda nakushukuru sana.