Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Mheshimiwa Rais, Makamu wa Rais na Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa jinsi ambavyo wameendelea kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi kupitia Wizara hii, hakika naiunga mkono Tanzania mpya ya viwanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza sana Waziri mwenye dhamana na kwa weledi mkubwa, juhudi na jinsi anavyojituma kupitia Wizara hii, hakika ni Waziri mchapakazi. Pia niipongeze sana timu ya Wizara kwa jinsi ya utendaji wao na kuwapatia Watanzania tumaini la viwanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, kiwanda cha General Tyre, naomba ufafanuzi wa kina wa kiwanda cha General Tyre kwani maelezo yanayotolewa ama maelekezo ambayo yamekuwa yakitolewa ndani ya Bunge hili na maelezo ya hotuba ya leo yanakinzana. Maelezo kuhusu Kiwanda cha General Tyre kwenye Hotuba za bajeti kwa miaka 2015/2016 na 2016/2017 ni tofauti (kila mwaka yanaletwa maelezo mengine mapya. Naomba ufafanuzi wa kina, maelezo gani ni sahihi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa mtoa hoja anifafanulie wakati anahitimisha hoja yake.