Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu MPM - Kiwanda cha Karatasi Mgololo. Mara kadhaa nimeongea na Mheshimiwa Waziri kuhusu kiwanda hiki na hata nimefikia kumwandikia, kuomba ridhaa ya kuuona na kuupitia mkataba wa ubinafsishaji wa kiwanda hicho ambacho awali kilijulikana kwa jina la SPM.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunapoenda uchumi wa viwanda jambo ambalo Serikali ilisisitiza ni kuhakikisha kuwa wote waliopewa viwanda kuhakikisha vinazalisha katika uwepo na malengo yaliyokusudiwa. Hata hivyo, MPM wanazalisha katika stage fulani kisha wanasafirisha material kwenda kufanya finishing Kenya, kisha karatasi zinarejeshwa kuja kuuzwa hapa nchini, hapa kuna double loss.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa, hawazalishi end product kwa maana ya karatasi, tunapoteza sehemu ya ajira kwa sehemu ya finishing kwenda kufanyiwa Kenya, lakini pia tunapoteza mapato maana tungeweza kupata fedha za ndani na kigeni kwa kuuza ndani na nje ya nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu ya masuala ya East Africa Community kuhusu rules of origin, MPM inatuletea karatasi kutoka Kenya na ushuru unaolipiwa is only 10% na siyo 25% maana sote tupo ndani ya EAC.

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri, kiwanda hiki kinauziwa magogo nusu ya bei 14,300/= kwa cubic meter, inapewa magogo hayo na Serikali (Sao Hill Forest). Je, kina sababu gani ya kutozalisha finished product kwa maana ya karatasi? Kusimamia na kuhakikisha kuwa ile machine Na.1 inafanya kazi italeta tija na kuipa Serikali heshima kuwa inamaanisha ilichosema kuwa, itahakikisha wote waliopewa viwanda wanatenda kadri ya malengo yaliyokusudiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, One Stop Centre, Uanzishwaji biashara za kati na za chini ni suala lenye malengo marefu kiasi kwamba inasababisha biashara nyingi kutokuwa rasmi. Ushauri, tuwe na one stop centre, mfano wa TIC kila Mkoa, kuliko ilivyo sasa mara BRELA, mara TIN, mara OSHA. Tuki-centralize katika level ya mkoa itarahisisha suala zima la kuanzishwa biashara.

Mheshimiwa Naibu Spika, kati ya masuala ambayo ukizungumza na Jumuiya ya Kibalozi (Diplomatic Community) ni suala la Double Taxation na Protection of Investments, wanasema mahusiano katika dunia ya sasa ni kuhusu kuimarisha fursa za kibiashara (Trade Opportunities) na ili kuzifaidi fursa hizo ni lazima pawepo mazingira bora ya kufanyia biashara na uwekezaji. Mazingira hayo mojawapo ni hili la double taxation na protection of investments.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nchi nyingi mfano Oman, Kuwait na za South East Asia, kama Korea, Japan na hata China ziko tayari kushawishi watu wao kuja kuwekeza hapa nchini, lakini ukakasi upo kwenye assurance yao hususani katika masuala hayo ya double taxation na protection of investments.

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wangu ni kwamba tupunguze woga, tupo na mashaka mno, kila jambo tunahisi tutaibiwa au kudhulumiwa, naamini tunao wataalam ambao watatufanya tufikie ile tunaita win win agreement. Hivyo ili yafanikiwe ni lazima Wizara ishirikiane na Wizara ya Mambo ya Nje na Wizara ya Fedha, ambao focus yao ni kukusanya tu pasipo kuangalia kuwa bila ushiriki wao katika suala zima la double taxation, itakuwa haileti tija iliyokusudiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu Maafisa Biashara. Katika mchango wangu bajeti iliyopita niligusia suala hili, kuwa tunapoenda uchumi wa viwanda na reflection yake kiuwekezaji kama lilivyo jina la Wizara, Muundo wa Kada hii kuendelea kufichwa ndani ya Idara ya Fedha katika Halmashauri zetu sio sahihi. Ikiwa Nyuki tu ni Kitengo kwa nini hii isifanywe Idara au angalau Kitengo?

Mheshimiwa Naibu Spika, Maafisa Biashara wamebaki kufanya kazi ya kukagua leseni, wapo vijana ni wasomi wazuri lakini wako under utilization, kwa sababu hata Wakurugenzi wanajikuta wanawapangia kazi ambazo sio za utaalam wao. Ni wakati sasa kada hii, ninyi Wizara muongee na Utumishi na TAMISEMI muweze kuipa nguvu kimuundo ili watumike ipasavyo hasa katika suala zima la biashara na uwekezaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mafinga Mjini na Uchumi wa Mazao ya Misitu (Mbao). Mji wa Mafinga ni kitovu cha shughuli za kiuchumi na uzalishaji katika Wilaya ya Mufindi na Mkoa wa Iringa. Hata hivyo watu hawa hawajapata fursa ya kupata huduma mbalimbali na changamoto wanazokutana nazo hasa katika sekta ya mbao, uzalishaji wa nguzo na milunda. Ombi langu, naomba waje hapa Dodoma kutokana na Waziri na Watendaji ili msikie maoni na ushauri wao kwa namna gani mnaweza kuwasaidia kushiriki ipasavyo katika suala zima la kuelekea uchumi wa viwanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu SIDO, inafanya kazi vizuri lakini SIDO wamejikita level ya Mkoani tu, Mafinga ina fursa yingi, tungependa SIDO ishirikiane na Halmashauri ya Mji wa Mafinga katika suala zima la kuwepo ama kutenga Industrial clusters kama walivyofanya Mkoa wa Mbeya.

Mheshimiwa Naibu Spika, Industrial Cluster’s, jambo hili lilijitokeza mwaka 2016/2017, hata hivyo nikifanya tathmini ni Halmashauri chache zimelitekeleza. Nashauri, kwa kushirikiana na TAMISEMI, Halmashauri zipewe maelekezo maalum kutenga maeneo hayo na ikibidi wapewe deadline maana hatuwezi kuwa na viwanda pasipo kutenga hizo Industrial Cluster’s.