Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, Napenda kuunga mkono hoja mapendekezo ya hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.

Mheshimiwa Naibu Spika, aseme ni lini ataenda Jimbo la Mlimba katika Kata ya Namwawala, Kata ya Mofu, Vijiji vya Idandu na Miyomboni ili kuweka utaratibu wa ujenzi na kilimo cha miwa ya sukari na wananchi waweze kunufaika ili kuwaondolea tabu wanazoendelea na kupata miaka mingi sasa bila kuwa na uongozi wa Serikali za Vijiji kwa kuwa ni eneo la uwekezaji wa kiwanda cha sukari.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Jimbo la Mlimba ni eneo la kilimo kikubwa cha mpunga, lakini Serikali haijaweka mkakati na uendelezaji wa wakulima kuongeza thamani ya mazao yao kwa kuwawezesha kuwepo kwa viwanda vya uchakataji.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.