Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Ussi Salum Pondeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chumbuni

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. USSI SALUM PONDEZA AMJADI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumpongeza Mheshimiwa Waziri kwa juhudi zake za kuiendeleza nchi katika sera ya Viwanda iliyowekwa na Mheshimiwa Rais John Pombe Joseph Magufuli kwa kutekeleza kwa vitendo, kwa kweli viwanda ni kitu muhimu sana kwa maendeleo ya nchi. Nakupongeza sana Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuomba sana Serikali yangu ya CCM kujaribu kulimaliza tatizo la Liganga na Mchuchuma kwa kuwalipa fidia wale wananchi wa Ludewa na kuendeleza yale machimbo na kumtafuta mwekezaji mwenye uwezo kwani ni muda mrefu sasa toka tuseme kuna mwekezaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili ni upatikanaji wa vibali vya uwekezaji wa haraka kwani TIC kuna urasimu sana na hivyo kupeleka wawekezaji kuondoka na kufanya uwekezaji kwenda na mwendo wa kusuasua, hivyo tutachelewa kufikia malengo ambayo tumejiwekea.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa haya machache, naunga mkono hoja.