Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Mheshimiwa Waziri kwa kazi nzuri ya kutekeleza adhma ya Serikali ya viwanda. Ombi, Mkoa wa Kagera tunasahaulika kwenye vipaumbele vya flagship projects hususan uanzishwaji wa viwanda vinavyoendana na comperative advantage za mkoa husika.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Waziri, wakati ana-wind up atueleze Wanakagera ni lini Serikali itasukuma uwekezaji wa kiwanda cha kusindika nyama ili kusaidia kutunza uchumi wa mkoa kwa kuwa unaongoza kwa wingi na ufugaji ng’ombe nchini. Kufanya hivi kutasaidia kutatua migogoro ya wakulima na wafugaji inayosababishwa na ng‘ombe wengi sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara itusaidie vijana wa Kagera hususani Wilaya ya Karagwe waweze kuwafikiria na SIDO‘s SME guarantee scheme.

Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru Mheshimiwa Waziri kwa kunisikiliza.