Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Lathifah Hassan Chande

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. LATHIFAH H. CHANDE: Mheshimiwa Naibu Spika, ni mwaka wa pili sasa tangu Serikali ya Awamu ya Tano ijinasibu kuwa hii ni Tanzania ya viwanda. Kwanza kabisa, napenda kuzungumzia juu ya rasilimali tulizonazo. Gesi asilia iligundulika kwa mara ya kwanza katika visiwa vya Songo Songo, Mkoani Lindi mwaka 1974. Ikagunduliwa Mtwara Vijijini (Mnazi Bay mwaka 1982 na Ntorya mwaka 2012), Mkuranga Mkoa wa Pwani mwaka 2007 na Lindi, Kiliwani mwaka 2008.

Mheshimiwa Naibu Spika, kiasi cha gesi asili iliyogunduliwa katika maeneo haya inakadiriwa kuwa futi za ujazo trilioni nane. Katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita kumekuwa na kasi kubwa ya utafutaji mafuta na gesi asilia uliojikita zaidi kwenye maji ya kina kirefu cha bahari na kiasi cha gesi asilia iliyogunduliwa katika kina kirefu cha maji ni takribani futi za ujazo trilioni 33.7. Jumla ya gesi asili iliyogunduliwa nchi kavu na baharini inafika takribani futi za ujazo trilioni 41.7. Rasilimali hii ya gesi asilia inaweza kutumika katika maeneo mbalimbali yakiwemo kuzalisha umeme, malighafi ya kuzalisha mbolea na kemikali, nishati viwandani, majumbani na kwenye taasisi mbalimbali.

Mheshimiwa Naibu Spika, mpaka sasa Mkoa wa Lindi hauna hata kiwanda kimoja cha kuzalisha mbolea za viwandani licha ya gesi kuwepo mkoani hapo. Ni wakati sasa wa Serikali kutafuta na kuelekeza wawekezaji wa kuzalisha mbolea katika Mkoa wa Lindi ukizingatia ukamilikaji wa barabara ya Masasi-Ruvuma kupitia Tunduru utafanya usafirishaji uwe rahisi wa mbolea hiyo hasa ukizingatia Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini ndiyo watumiaji wakubwa wa mbolea hiyo ya viwandani. Ujenzi huu wa viwanda utasaidia vijana wa Lindi ambao zaidi ya asilimia arobaini (40%) hawana ajira, jambo ambalo litapunguza kama si kuondoa kabisa tatizo la ajira kwa vijana Mkoani Lindi na Kanda ya Kusini kwa ujumla.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda pia kuzungumzia juu ya usindikaji na kuongeza thamani mazao. Mkoa wa Lindi unazalisha kwa wingi mazao kama korosho, ufuta, muhogo, mbaazi na mengine mengi. Kwa sasa duniani kote faida ya kilimo chochote kiko kwenye usindikaji na uongezaji thamani ya zao husika. Mkulima wa Lindi na Mtwara bado hajanufaika na anachokizalisha kwa kuwa mteja wake mkuu ni mlanguzi ambaye ananunua kwa mkulima na kuuza kwenye masoko na makampuni makubwa kwa bei itakayompa faida.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoani Lindi kulikuwa na viwanda vya korosho ambavyo vilikuwa na mashine za kubangua korosho lakini sasa viwanda hivi havifanyi kazi.

Matokeo yake korosho zinauzwa bila kuongezwa thamani na kupelekea kupunguza kipato. Naiomba Serikali ijikite katika kufufua viwanda hivi Mkoani Lindi na pia katika kujenga viwanda vingine hata kwa kushirikisha private sectors ili kuweza kumnufaisha mkulima, kutoa ajira kwa vijana, kudhibiti walanguzi na hatimaye kuongeza pato la Taifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, tulikuwa na viwanda vya nguo hapa nchini, vipo wapi sasa? Mitumba leo inapigwa marufuku huku Serikali haijaleta njia mbadala wa kuleta nguo za bei nafuu kuweza kukidhi mahitaji ya majority. Makubaliano ya East African Common Market ni kwamba mitumba marufuku ikifika 2019. Wenzetu Rwanda wameanza kuwapa mafunzo akinamama kutengeneza nguo za gharama nafuu kwa kutumia materials zinazopatikana kwa wingi. Imebaki miaka miwili tu tutapiga marufuku mitumba ya Ulaya badala yake tutanunua za bei rahisi kutoka Rwanda na China. Sisi tutanufaika na nini?

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna kiwanda Morogoro kinaitwa Mazava ambacho kinazalisha sport wear lakini bidhaa zote zinapelekwa Ulaya na Marekani wakati Tanzania hakuna product yoyote sokoni. Tunahitaji kuwa na viwanda vya nguo vitakavyoweza kuzalisha, kujiendesha pia wakati huo huo nguo ziweze kuuzwa kwa bei nafuu. Tukiwa na viwanda vyetu vitakavyozalisha kwa wingi itasaidia kushusha gharama za uzalishaji na bei ya kuuza itakuwa rahisi na mwananchi wa kawaida ataweza kumudu.

Mheshimiwa Naibu Spika, wenzetu Kenya wana kitu kinaitwa Vision 2030. Kwenye manufacturing wana-target kutoka kwenye kumiliki soko kwa 7% hadi kufikia 15% ambayo ni zaidi ya mara mbili. Kwa maana hiyo viwanda walivyonavyo sasa wataviongeza mara mbili. Kipaumbele kimoja cha Wizara ya Viwanda na Biashara Kenya ni kutengeneza skilled technical human resources.

Mheshimiwa Naibu Spika, moja kati ya vitu vinavyoangusha watu wetu hapa hawana uwezo wa kushindana kimataifa, skill level iko chini. Kwa hiyo, hata tukijenga viwanda bila kuwa na programu maalum ya kunyanyua skill za watu wetu, bado effect kwenye uchumi wa viwanda itakuwa ndogo maana kazi zitakuja kuchukuliwa na watu wa mataifa ya jirani ambao wameandaliwa Kenya na Rwanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kushauri Serikali ijikite katika kujenga viwanda na vilevile kutayarisha vijana kwa kutengeneza skilled technical human resources ili waweze kupata ajira katika hivi viwanda. Vilevile Serikali iboreshe miundombinu ili kuwezesha movement ya bidhaa zinazotengenezwa, maana kuongelea Tanzania ya Viwanda bila kuwa na uhakika wa miundombinu ya barabara ni sawa na kuongelea mwili wa binadamu bila damu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nawasilisha.