Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Ahmed Mabukhut Shabiby

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Gairo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. AHMED M. SHABIBY: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kutoa pongezi za dhati kwa Wizara hii na kwa viongozi wake wote. Natambua Wizara hii ni kiungo muhimu kati ya wafanyabiashara na Serikali. Bila Wizara hii kufanya kazi kwa umakini na uweledi, basi ndoto ya Serikali yetu ya kuwa na viwanda itakuwa ndoto isiyotimia. Kwa sababu kumekuwa na kila aina ya matamko na sheria za ovyoovyo za kuua biashara ndani ya nchi hii hasa kutoka katika mamlaka zilizopo kama EWURA, TBS, NEMC, SUMATRA na zinginezo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano, ili mtu apate leseni ya NEMC ya Petrol Station, kwanza lazima apate consultant ambaye amepitishwa na NEMC na baada ya hapo asajili mradi, consultant pekee analipwa shilingi millioni saba (Sh.7,000,000/=) na kusajili mradi napo fedha. Ukimaliza consultant, ili watu wa NEMC waje kukagua ripoti ya consultant nao unalipa gharama zao za kuja site.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya hapo wakiridhika kukupa leseni, unalipa shilingi milioni kumi (Sh.10,000,000/=) na baada ya hapo utaendelea kulipa ada ya kila mwaka shilingi laki tatu (Sh.300,000/=). Utakuta inagharimu zaidi ya shilingi milioni ishirini na tano kupata Leseni ya NEMC kwa kituo kimoja na bila kujali kipo kijijini au mjini. Je, kwa faida ya Sh.90 kwa lita kuna biashara hapo, bado gharama za kodi, upungufu wa mafuta, mishahara na kadhalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, hii nimetoa mfano kwa kituo cha mafuta lakini ndiyo hivyo hivyo kwa hoteli au viwanda ukitaka kupata leseni ya NEMC. Kwa mfano huu mdogo, Wizara hii inachukua hatua gani kuhakikisha mamlaka zilizopo zinafanya kazi zake kwa ufanisi na siyo kuwa wakusanya faini na watoza kodi au Wizara hii ni jina tu? Kwa nini chochote kinachofanywa na mamlaka kuhusu biashara ndani ya nchi hii kisihusishe Wizara kwanza kabla ya sheria na kanuni zao?

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba majibu.