Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Kasuku Samson Bilago

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Buyungu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuchangia kwenye sekta ya viwanda kama ifuatavyo:-

(i) Serikali itafute wawekezaji wa kufufua viwanda vilivyotaifishwa na Serikali na kuwakabidhi wawekezaji wazawa ambao wameshindwa kuviendeleza.

(ii) Serikali itafute wawekezaji kwenye viwanda vidogo vya matunda, viungo (nyanya - tomato sauce), viwanda vya juisi za machungwa, maembe, nanasi (simple machines) kwenye maeneo yanayozalisha matunda ya nyanya na pilipili.

(iii) Viwanda vinahitaji umeme wa kutosha na wenye uhakika na wa gharama nafuu. Haiingii akilini kuwa na umeme wa gharama kubwa wakati tunazalisha kwa gesi ya Mtwara.

(iv) Kuimarisha sekta ya kilimo kutasaidia upatikanaji wa rasilimali/malighafi za viwanda. Hivyo basi kilimo endelevu ni cha kumwagilia na matumizi bora ya pembejeo. Agriculture - Raw materials - Industrial goods/ product.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu biashara napenda kuchangia yafuatayo:-

(i) Biashara zinafungwa nchini kwa sababu ya mazingira ya kufanya biashara kutokuwa rafiki. Serikali inawabana sana wafanyabiashara kwa kuweka kodi nyingi sana za uingizaji wa bidhaa toka nje. Hii ni hatari kwa uchumi.

(ii) Mfanyabiashara mpya na hasa wale wadogo wanawekewa makadirio makubwa ya kodi TRA hata kabla hajaanza kuzalisha. Serikali iruhusu waanze biashara kwanza kisha itoze kodi tena inayokubalika.

(iii) Leseni za biashara ndogo hazitolewi mpaka mfanyabiashara akalipe kodi TRA apewe tax clearance ndipo akakate leseni ya biashara Halmashauri. TRA hawako efficient/ available hasa vijijini kama Wilaya ya Kakonko, hawapo mpaka mfanyabiashara aende Kibondo, Mtambo wa TIN haupo Kakonko wala Kibondo mpaka Kigoma sawa na km.300. Hivyo wafanyabiashara wanashindwa kwenda Kigoma (300km) ili kupata TIN number. Nashauri wafanyabiashara hawa wakate leseni za biashara za Halmashauri ili nazo zipate fedha wakati TRA ikiweka utaratibu wa kutoa TIN vijijini.

(iv) Machinga kuuza bidhaa zao holela hasa maeneo ya Kariakoo soko la wafanyabiashara wakubwa. Hii ni kwa sababu wao hawalipi kodi hivyo huchukua bidhaa za wafanyabiashara dukani na kuziuza bila ushuru wowote. Hivyo wenye maduka Kariakoo hawalipi kodi kwani bidhaa zao zinauzwa nje na machinga, kwa sababu zina bei ndogo na wenye maduka kutotumia EFD machines.

Mheshimiwa Naibu Spika, upande wa wawekezaji, nashauri wapewe masharti nafuu ili wahamasike kuja kuwekeza nchini. Mazingira rafiki na ya kuvutia yatawakaribisha wengi, invite more coming on board.

Mheshimiwa Naibu Spika, nawasilisha.