Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, Ukerewe ni moja kati ya maeneo ambayo yana rasilimali za kutosha kwa ajili ya malighafi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na uzalishaji mkubwa wa samaki na matunda (mananasi, machungwa na maembe), Wizara ielekeza wawekezaji kwa ajili ya viwanda vya kuchakata samaki na matunda katika eneo hili ili kuokoa matunda mengi kuharibika kwa kukosa soko. Jambo hili litasaidia pia kukuza uchumi wa wananchi hasa vijana na akinamama kwenye visiwa hivi vya Ukerewe.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia kutokana na uzalishaji mkubwa wa samaki katika Visiwa vya Ukerewe, litakuwa jambo lenye maslahi kwa Taifa iwapo vitajengwa viwanda vya kuchakata samaki kwenye maeneo haya badala ya kuwasafirisha kuwapeleka katika maeneo mengine.

Mheshimiwa Naibu Spika, nawasilisha.