Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Naibu Spika, nchi yetu imedhamiria kuwa nchi ya uchumi wa kati ambao unategemea uimarishaji wa viwanda. Tanzania tulikuwa na viwanda vingi miaka ya nyuma lakini tulifika mahali tukauza au kuvibinafsisha vingine, tena kwa bei ndogo sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, naishauri Serikali kurudi nyuma katika kipindi kile cha uuzaji wa viwanda, kuangalia mikataba ile yote ili kubaini ni vipi tunaweza kurejesha viwanda mikononi mwa Serikali. Ujenzi wa viwanda ni ghali sana na ni bora na rahisi kufufua vile vya zamani kuliko kuweka viwanda vipya.

Mheshimiwa Naibu Spika, viwanda maana yake ni ajira kwa vijana wetu. Serikali hii ina mipango mizuri kwenye makaratasi, lakini kwa kweli kiuhalisia bado kabisa viwanda havionekani.

Mheshimiwa Naibu Spika, naishauri Serikali kuanzisha viwanda vile ambavyo malighafi yake inaweza kupatikana nchini. Tunayo mazao ya mashambani, tunayo mifugo mingi sana na pia tunayo madini mengi. Viwanda pia vilenge katika kukuza uzalishaji wa mazao hayo ya hapo juu. Ni jambo la kuhuzunisha, kwani mazao yanalimwa hapa nchini lakini yanasindikwa nje. Mfano, nchi yetu inazalisha korosho nyingi lakini inabanguliwa nje. Huku ni kukosesha Watanzania ajira na pia kupoteza mapato ya Serikali.