Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

Hon. George Mcheche Masaju

Sex

Male

Party

Ex-Officio

Constituent

None

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa nami niweze kuchangia, lakini pia namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa fursa hii. Yapo mambo kadhaa yamezungumzwa hapa ya Kikatiba na Kisheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwanza niseme hivi; Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 inatoa haki za msingi, lakini na wajibu. Hivi vitu vinakwenda pamoja; haki na wajibu.

Katiba hiyo hiyo ndiyo inayoipa Bunge mamlaka ya kusimamia na kuishauri Serikali. Ibara ya 100 ina vifungu viwili; cha kwanza na cha pili. Kimoja kinatoa uhuru wa majadiliano, lakini kifungu kidogo cha pili kinasema, bila kuathiri masharti ya Katiba hii na Sheria na huo ndiyo msingi wa kanuni ya 64.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba kuwakumbusha Waheshimiwa Wabunge Ibara ya 29(5) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano inasema hivi;

“Ili watu wote waweze kufaidi haki na uhuru vilivyotajwa katika Katiba hii, kila mtu ana wajibu wa kutenda na kuendesha shughuli zake kwa namna ambayo hataingilia haki na uhuru wa watu wengine au maslahi ya Umma.”

Mheshimiwa Mwenyekiti, yamezungumzwa mambo hapa ambayo kimsingi yanawadhalilisha Wanajeshi na Jeshi la Wananchi wa Tanzania. Bunge lisiruhusu hiki kitu. Bunge limetunga Sheria; tunayo Sheria ya Usalama wa Taifa (The National Security Act) na sheria hii, Kifungu cha (4) inataja “Public officer” ikiwajumuisha na Wabunge. Yako mambo ambayo huwezi ukayasema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kifungu cha (4) cha Sheria ya The National Security Act; na hata kama umeambiwa hizo habari, ndiyo maana tuna fursa hapa za kuchangia hata kwa maneno na kwa maandishi kwa sababu haya mambo yapo protected. Someni Kifungu cha (4) cha Sheria ya Usalama wa Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais Kikwete enzi zake aliwahi kutuambia; “akili za kuambiwa, changanya na ya kwako.” Hamwezi mkazungumza mambo ambayo hata yanadhalilisha wanawake wa Wanajeshi; Hao Wanajeshi wenyewe wako humu halafu tunakaa kimya!

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, mimi nilikuwa nataka kusema hivi…

T A A R I F A . . .

MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, hii taarifa naikataa. Yeye alikusudia kueleza tu mamlaka. Nimesema hapa, Ibara ya 100(2) inasema:

“Bila kuathiri Katiba hii au masharti ya Sheria nyingine yoyote inayohusika.”

Nimesema hivi, Katiba yetu inatoa haki na wajibu. Kwa mfano, huwezi ukapiga mtu au ukatukana mtu, ukasema nina uhuru wa hapa. Haiwezekani! Tunatambua Katiba inatoa mamlaka hayo na tumetunga sheria hizi hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nami ngoja niwashauri hapa. Najua hapa wakati fulani mnapotoshwa. Uhuru huo mnaotafsiri Katiba vibaya, kuna siku nyingine mtajikuta pabaya, that is it! Eeh! (Kicheko/Makofi)

Hamuwezi, kwa sababu Katiba iko wazi, nakupeleka tu Mahakamani. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, aliyasema; lakini ninachotaka kusema ni hivi, Waheshimiwa Wabunge watumie uhuru wao kuishauri na kuisimamia Serikali kwa hekima. Eeh! Haya mambo yapo hapa. Siku hizi wameanzisha utaratibu yale unayoyakataa, wanaweka kwenye mitandao. Wakiweka kwenye mitandao, nitawachukulia hatua za kisheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hawawezi kuwa protected.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nasimamia ununuzi hata Mikataba yote inapita hapa, vifaa vya kisasa wananunua; unaweka maneno hayo, una-expose Taifa hili kwa watu wengine kwamba Jeshi la Tanzania lina vifaa duni, kwa hiyo tunaweza tukaenda tukawavamia kule. Haiwezekani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, limezungumzwa hapa na kukubali kwamba Katiba Ibara 147 imepiga marufuku Wanajeshi kujiunga na Vyama vya Siasa. Hiyo ni kweli kwa sababu ni sharti kabisa la Kikatiba lakini, Ibara ya 45, Kifungu cha 25 cha Sheria ya Ulinzi wa Taifa (The National Defence Act) kimetoa Mamlaka kwa Rais ku-second mtu yoyote.

Kipindi chote hicho, huyo mtu anaendelea kuwa Mwenyekiti. Sasa kwa mfano, kama ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya au Mkuu wa Mkoa, tunajua yuko Mwenyekiti wa Chama wa Mkoa; Mwenyekiti wa Chama wa Wilaya ana majukumu yake, hawezi kuchukuliwa na Mkuu wa Mkoa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Katiba yenyewe ya Chama cha Mapinduzi imesema kwenye Ibara ya 94 na Ibara ya 80; “Mkuu wa Mkoa atakuwa Mjumbe wa hizo Kamati kama anatokana na Chama cha Siasa.” Eeh, na wote tunafahamu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwa sababu huyu anakwenda kufanya mambo ya Serikali kule siyo ya Chama. Katiba iko wazi. Huyu anatokana na Chama cha Siasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.