Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

Hon. Dr. Susan Alphonce Kolimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia Hotuba ya Mheshimiwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, lakini nitakwenda kwenye hotuba iliyotolewa na Kambi ya Upinzani katika ukurasa ule wa 14 ambapo walikuwa wanazungumzia suala la usalama wa mipaka ya nchi na hasa mgogoro wa mpaka wa Ziwa Nyasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nitoe taarifa ifuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuanzia mwaka 2014 tarehe 20 mpaka tarehe 21 Machi, mkutano wa kwanza ambao unasimamiwa na jopo la Marais wastaafu watatu ulifanyika. Nataka tu nitoe status kwa sababu swali lao linaulizia status, lakini sitaweza kuwaambia yale ambayo yanazungumzwa ndani ya jopo lile kwa sababu bado linaendelea na linatoa taarifa kwenye ngazi maalum inayohusika lakini sio mahali ambapo ni pa wazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda pia kulikumbusha na kuliambia Bunge lako Tukufu kwamba mahusiano ya Tanzania na Malawi yako vizuri, ninyi ni mashahidi na yako vizuri kwa ushahidi wa kwamba sisi kama Wizara ya Mambo ya Nje na kwa niaba ya Serikali tumeweza kufanya mikutano na Malawi kwa pamoja na yapo vizuri katika mahusiano ya kiuchumi na kijamii na ninyi ni mashahidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukienda katika suala la mgogoro wa mpaka wa Ziwa Nyasa, niseme tu kwamba, mgogoro ule ulisitishwa mwaka 2014 na sababu ya kusitishwa mgogoro ule ni kwamba Malawi ilikuwa unaingia kwenye uchaguzi mwezi Julai na kwa hiyo, Mwenyekiti wa jopo lile la usuluhishi akaona kwamba ni hekima Malawi wangekuwa hawana nafasi ya kuweza kuhudhuria vikao vile kwa hiyo, wakasitisha. Ilipofika mwaka 2015, Tanzania iliingia pia kwenye uchaguzi Mkuu, kwa hiyo, Mwenyekiti wa jopo pia alisitisha mazungmzo ya kujadili usuluhishi wa mgogoro huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa hivi nchi zote hizi haziko kwenye uchaguzi na utaratibu sasa hivi unafanyika ili kuweza kuendelea na mazungumzo haya katika mwaka huu. Kwa sasa hivi Mwenyekiti wa jopo hili anajaribu ku-consult na wadau watakaohusika katika Mkutano huu ili kuweza kuendelea na mazungumzo ya usuluhishi. Hiyo ndiyo status ya mgogoro huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu kwamba, naomba sana kwa Waheshimiwa Wabunge pamoja na Watanzania kwa ujumla wake, diplomasia iachwe ifanye kazi yake. Tunapokuwa tunaiingilia kwa kuangalia labda mitandao au nani kasema nini, nasema kwa niaba ya Wizara yangu kwamba jambo hili linashughulikiwa na lipo katika mikono ya jopo na tuiache diplomasia ifanye kazi yake. Hii ni kwa nia njema tu, kwa sababu tunapokuwa tunashabikia kuchukua maneno yanayosemwa huku, sisi tunasema kutoka kwenye Ofisi husika kwamba usuluhishi wa jambo hili unaendelea na hivi karibuni mtaambiwa lini watakapo- consult kwamba wadau watakuwa na nafasi kwa siku gani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la mipaka; kuna Kamati ambayo inaendelea kufanya kazi yake, lakini kama mnavyojua kwamba mpaka wa Ziwa Nyasa bado haujaweza kupata usuluhishi wa kusema kwamba mpaka unapitia wapi mpaka hapo usuluhishi utakapokuwa umekwisha, jopo litakapomaliza kazi yake ndipo mpaka wa Ziwa Nyasa utakapokuwa umesemwa. Kwa hiyo, siwezi kuzungumzia suala la mpaka kama lilivyoandikwa kwenye hotuba ya Kambi ya Upinzani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile kwenye hotuba ile ile ya Kambi ya Upinzani, katika ule ukurasa wa 15, Kambi ya Upinzani inauliza ni nini hatima ya mgogoro huu? Hivi kweli tunaweza tukatoa jibu saa hizi, kama mgogoro huu unaendelea kujadiliwa na usuluhishi wake unaendelea! Wawe na subira, Kamati hiyo na jopo litakapomaliza kazi yake, ndipo tutakapojua kwamba lini tutapata jibu na mwisho wa mgogoro.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema haya, naomba kuunga mkono hoja hii.